Search This Blog

Friday, September 6, 2013

TFF YAOMBWA KUWATUMIA VIBALI WANASOKA WA TANZANIA NCHINI AFRIKA KUSINI.

Vijana wawili raia wa Tanzania wanaocheza soka la kulipwa nchini Afrika Kusini wamesikitishwa na kitendo cha Shirikisho la soka nchini TFF kushindwa kuwatumia ITC walizoziomba takribani wiki moja sasa,
Vijana hao Mohamed Ally Ibrahim (18 )  na Robert Titus Kobelo (21 ) wanaombewa vibali na timu ya CACADU UNITED FC inachoza ligi daraja la pili ya nchini Afrika Kusini,
ligi hiyo inayodhaminiwa na kampuni ya simu za mikononi ya VODACOM.
Vijana hao ni zao la JAKI ACADEMY ya Mbagala jijini Dar Es Salaam wanataka kujiunga na timu hiyo yenye maskani yake kwenye kitongoji cha Alexandria huko mjini Port Elizabeth.

Mmoja wa wakurugnzi wa timu hiyo ndugu BONGANI MASHIBO wakati Akiongea na Blog hii amesema
'' Nasikitika sana mpaka sasa hatujapata jibu toka TFF,Tangu tumewaombea vibali hawa vijana,kila tukiwasiliana nao wanasema wanatuma lakini hawatumi,kama unaweza nenda kawasisitize TFF watutumie hivyo vibali ''.

     Hawa  ndio vijana wanaomba vibali vya kucheza nchini AFRIKA KUSINI.


  Mkurugenzi wa timu ya CACADU UTD BONGANI MASHIBO.

No comments:

Post a Comment