Search This Blog

Thursday, August 15, 2013

YANGA SC VS AZAM FC JUMAMOSI HII - VIINGILIO HIVI HAPA

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom, Yanga na makamu bingwa Azam wanavaana keshokutwa (Jumamosi) kwenye mechi ya Ngao ya Jamii (Community Shield) kuashiria uzinduzi wa msimu mpya wa 2013/2014.

Mechi hiyo inayotarajiwa kuwa kivutio kwa wapenzi wa mpira wa miguu nchini itachezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10.30 jioni ambapo mshindi atakabidhiwa ngao.

Iwapo dakika 90 za mechi hiyo hazitatoa mshindi, timu hizo zitatenganishwa kwa mikwaju ya penalti huku asilimia 10 ya mapato ya mechi hiyo yakienda kwa kituo cha kulelea watoto cha SOS.

Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 7,000 kwa viti vya rangi ya kijani na bluu wakati viti vya rangi ya chungwa ni sh. 10,000. Watakaiongia viti vya VIP C watalipa sh. 15,000, viti vya VIP B ni sh. 20,000 wakati VIP A watalipa sh. 30,000.

LIGI DARAJA LA KWANZA KUANZA SEPT 14
Michuano ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) inayoshirikisha timu 24 zilizogawanywa katika makundi matatu msimu huu (2013/2014) itaanza kutimua vumbi Septemba 14 mwaka huu.

Kila timu itakayoongoza kundi lake katika ligi itakayochezwa kwa mikondo miwili (nyumbani na ugenini) ndiyo itakayopanda daraja kucheza Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu wa 2014/2015.

Mechi za ufunguzi kwa kundi A zitakuwa kati ya Tessema vs Green Warriors (Uwanja wa Karume, Dar es Salaam) wakati Septemba 15 mwaka huu ni Transit Camp vs Polisi Dar (Uwanja wa Mabatini, Pwani), Ndanda vs Friends Rangers (Uwanja wa Nangwanda, Mtwara) wakati Villa Squad vs African Lyon itachezwa Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.

Kundi B ni Burkina Faso vs Polisi Moro (Uwanja wa Jamhuri, Morogoro), Mkamba Rangers vs Lipuli (Uwanja wa CCM Mkamba, Morogoro), Majimaji vs Mlale JKT (Uwanja wa Majimaji, Songea) wakati Septemba 15 mwaka huu Kimondo SC vs Kurugenzi (Uwanja wa Sokoine, Mbeya).

Mechi za ufunguzi kundi C ni Polisi Mara vs Polisi Dodoma (Uwanja wa Karume, Musoma), Kanembwa JKT vs Polisi Tabora (Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma), Stand United vs Mwadui (Uwanja wa Kambarage, Shinyanga), na Pamba vs Toto Africans (Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza).

Mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo utamalizika Oktoba 26 mwaka huu wakati wa pili utamalizika Machi 22 mwakani.

1 comment:

  1. SAKATA LA YANGA NA AZAM MEDIA:HIKI NDICHO KILICHOJIRI KWENYE KIKAO KILICHOITISHWA NA SERIKALI
    Nyeti za kikao kilichoitishwa jana na Naibu waziri wa habari vijana utamaduni na michezo Amos Makalla kujadili mkataba wa Azam Media kuonesha mechi za ligi kuu ambao umegomewa na Yanga zimevuja.
    Supermariotz imenasa mambo yalivyokwenda ndani ya kikao hicho na kile kilichopitishwa.
    Shuka nayo :
    Yanga walikuwa na madai ama hoja nne kwenye kikao hicho : Madai ya Yanga
    1. Mgao wa pesa zaidi ya timu nyingine
    2. Azam TV wanyimwe haki kwa kuwa wana timu ligi kuu
    3. Kamati ya ligi haina mamlaka kisheria kwa hiyo mkataba uvunjwe
    4.Mchakato(Tendaring) haikufanywa kwa uwazi kwa hiyo urudiwe tena
    Kwenye kikao hicho mengi yalijadiliwa lakini hiki ndio ambacho kilipatikana baada ya majadiliano ya muda mrefu kutoka kwa wajumbe mbalimbali waliohudhuria wakiwemo viongozi wa Azam Media,viongozi wa Yanga,viongozi wa kamati ya ligi,viongozi kutoka wizarani,viongozi wa TFF na wajumbe kutoka vilabu vya ligi kuu.
    MAJIBU
    1. Mgao wa pesa zaidi ya timu nyingine haiwezekani na mgao unabaki palepale lakini Yanga wameshauriwa wakutane na Azam Media,na ikabainika kwenye kikao hicho kuwa ni kitu ambacho tayari kilichafanyika na walipewa ofa kama ya Simba lakini waliikataa lakini mbele ya kikao hicho wamelazimika kuikubali.

    2. Hoja yao ya kutaka Azam TV wanyimwe haki kwa kuwa wana timu ligi kuu ambayo ni Azam FC imeshindikana na makubaliano ni kwamba Azam FC itaendelea kucheza ligi kuu na Azam Media wataonesha ligi kuu,na Kamati ya ligi imewaambia Yanga watoe mwanasheria ili ashiriki kwenye mkataba na imebainika kuwa ni hoja ambayo waliambiwa tokea zamani na vilabu vyote waliambiwa kama kuna mwenye mwanasheria wa mikataba kama hiyo ampeleke,Yanga hawakupeleka.

    3. Hoja ya Kamati ya ligi kuwa haina mamlaka kisheria kwa hiyo mkataba uvunjwe imeonekana kuwa kamati ya ligi ina mamlaka kwahiyo hoja yao haina mashiko

    4. Hoja ya kwamba mchakato(Tendaring) haikufanywa kwa uwazi kwa hiyo urudiwe tena imeonekana Yanga hawana hoja kwakuwa kila kitu kilikuwa wazi na SuperSport walishiriki wakashindwa na bado kuna uwazi mpaka sasa kwakuwa MoU(Memorandum of Understanding) ambayo wamesaini inaruhusu kama yupo mshindani mwenye hela zaidi ajitokeze na mpaka sasa hakuna mshindani aliyejitokeza wa kutoa fedha zaidi ya hizo zaidi ya bilioni 5.5 zitakazotolewa na Azam Media katika miaka yao mitatu ya mkataba.
    Hayo ndiyo yaliyojiri kwenye kikao hicho,soma,tafakari na jibu utalipata.

    ReplyDelete