Search This Blog

Friday, August 30, 2013

OFFICIAL: TFF NA AZAM MEDIA WASAINI MKATABA WA BIL.5.5 KUONYESHA MECHI ZA LIGI KUU - AZAM TV KUANZA MWEZI UJAO

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na kampuni ya Azam Media leo (Agosti 30 mwaka huu) wamesaini mkataba wa haki za kipekee za televisheni (exclusive rights) utakaoiwezesha Azam TV kuonesha mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL).

Mkataba huo wa miaka mitatu wenye thamani y ash. 5,560,800,000 umesainiwa kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. Makamu wa Rais, Athuman Nyamlani amesaini kwa niaba ya TFF wakati aliyesaini kwa upande wa Azam Media ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo Thys Torrington.

Ligi Kuu ya Tanzania sasa itakuwa ikipatikana kupitia kisimbuzi (decorder) cha Azam TV kitakachokuwa na chaneli zaidi ya 50. Mechi hizo zinatarajiwa kuoneshwa moja kwa moja wakati wowote kuanzia mwezi ujao.

Makamu wa Rais wa TFF, Nyamlani amesema udhamini huo wa televisheni ni fursa pana kwa klabu kwani zitaweza kujitangaza zaidi huku wachezaji nao wakipata soko zaidi za mpira wa miguu.


2 comments:

  1. MMmm Yanga vipi jama!!wataonekana kwenye kioo au msimamo palepale?mtujuze jamani tulioko namtumbo,nanjilinji,kwangulelo, etc.

    ReplyDelete
  2. hawataonekana watapatikana zuku

    ReplyDelete