Search This Blog

Friday, August 30, 2013

HATIMAYE MAROUNE FELLAINI AOMBA KUONDOKA EVERTON BAADA YA MAN UNITED KURIPOTIWA KUONGEZA DAU

Marouane Fellaini amemwambia kocha wake Roberto Martinez kwamba anataka kuondoka Everton.
Uamuzi huo wa Fellaini unakuja baada ya Manchester United kuongeza dau lao kwa mbelgiji huyo - na beki wa kushoto wa timu hiyo Leighton Baines — mpaka kufikia £36million.
Fellaini, 25, bado hajapeleka ombi rasmi la kuhama lakini ameomba kwa maneno kuruhusiwa kujiunga na klabu ya Manchester United. 

Everton tayari wameshakataa ofa ya £26 million kutoka kwa kocha wao wa zamani, David Moyes. Lakini ofa mpya ya United imeongeza presha kwa klabu ya  Merseyside kuwauza nyota wake zikiwa zimebaki siku tatu kabla ya dirisha la usajili kufungwa.

No comments:

Post a Comment