Search This Blog

Friday, August 30, 2013

GARETH BALE AFIKIA MAKUBALIANO MASLAHI BINAFSI NA REAL MADRID

Gareth Bale amefikia makubaliano ya maslahi binafsi na Real  Madrid kuelekea uhamisho utakaovunja rekodi ya dunia kutoka  Tottenham.
Pamoja na hilo lakini miamba ya soka ya kihispania bado kwenye mazungumzo ya mwisho na Spurs juu ya ada ya uhamisho wa  £86m .
"Wakati mazungumzo yakiendelea jijini Madrid, tayari mchezaji ameshakubaliana maslahi binafsi na klabu," amesema mwandishi mkuu wa habari za michezo wa BBC Dan Roan.
. "Kilichobakia sasa ni Spurs kukubali rasmi ofa ya Real Madrid ambayo watalipwa kwa vipande katika muda wa miaka minne."

1 comment: