Search This Blog

Friday, August 30, 2013

ARSENAL HATA KAMA WANGEFUNGWA NA FENERBAHCE - BADO WANGEWEZA KUCHEZA LIGI YA MABINGWA WA ULAYA

Klabu ya soka ya Uturuki, Fenerbahce, imepigwa marufuku ya kushiriki katika michuano ya bara Ulaya msimu huu, baada ya mahakama ya upatanishi ya michezo CAS, kuidhinisha uamuzi uliokuwa umetolewa na shirikisho la UEFA kuwa klabu hiyo ilihusika na sakata ya kupanga matokeo ya mechi.

Klabu hiyo ilikuwa, tayari kujiunga na ligi hiyo ya UEFA Cup, baada ya kuondolewa na Arsenal katika michuano ya kuwania kombe la klabu bingwa barani Ulaya.
Shirikisho la UEFA, liliipiga marufuku Fenerbahce mwezi Juni mwaka huu, baada ya kuwapata maafisa wa klabu hiyo na hatia ya kupanga matokeo ya mechi ili kushinda ligi kuu ya soka nchini Uturuki.

Kwa maana hiyo hata kama wangefanikiwa kuitoa Arsenal katika mechi ya kufuzu champions league isingekuwa na maana kwao kutokana kufungiwa huko.

1 comment: