Search This Blog

Thursday, July 4, 2013

VAN GINKEL MCHEZAJI WA PILI KUSAJILIWA NA JOSE MOURINHO TANGU ATUE CHELSEA - ANGALIA UJUZI WAKE

JOSE MOURINHO amefanya usajili wa pili tangu kujiunga na Chelsea kwa kumsajili kiungo wa kidachi Marco van Ginkel.

Chelsea wamethibitisha asubuhi hii kwamba wamekubaliana ada ya uhamisho, ambayo inaaminika kufikia kiasi cha  £8million, na klabu ya Vitesse Arnhem kwa kwa ajili ya kupata saini ya kiungo huyo anayesifiwa mno na wachambuzi wa soka barani ulaya.

Kilichobaki sasa ili kukamisha usajili huo ni kwa Van Ginkel kufanyiwa vipimo vya afya na makubaliano ya maslahi binafsi, ingawa haya hayaonekani kuja kuwa kikwazo.

MUANGALIE VAN GINKEL HAPA


No comments:

Post a Comment