Search This Blog

Wednesday, July 31, 2013

SAKATA LA YANGA KUPINGA MECHI ZAO KUONYESHWA AZAM TV - WANACHAMA WA KLABU HIYO WAUNGA MKONO UONGOZI

Uongozi wa matawi wa klabu ya Yanga (wenyeviti na makatibu) leo umefanya kikao katika makao makuu ya klabu mtaa wa twiga/jangwani kisha kutoa tamko lao kwa waandishi wa habari kuhusiana na tamko la uongozi (kamati ya utendaji) kutokubali kuonyeshwa kwa michezo yake kwenye luninga.
Awali klabu ya Yanga juzi kupitia kamati ya utendaji ilifanya mkutano na waandishi wa habari juu ya mustakabali wa klabu kuhusiana na kutoridhishwa na kamati ya muda ya Ligi (TPL) kuingia makubaliano ya kurushwa matangazo ya televsheni kwenye michezo yake.
Akiongea na waandishi wa habari leo katibu mkuu wa Yanga Lawrence Mwalusako alisema baada ya kukaa na viongozi wa matawi ya klabu ya Yanga jijni Dar es salaam kwa pamoja wamekubali na kuunga mkono hoja zilizowasilisha na viongozi juu ya haki ya matangazo.
Mmoja wa viongozi wa matawi Bakili Makele akiongea kwa niaba ya viongozi wa matawi, alisema TFF inaamua kukandamiza soka la Tanzania kwa kuviamulia maamuzi yake juu ya kuonyeshwa kwa michezo ya timu kwenye luninga.
Makele amesema taratibu za kuipa kampuni ya Azam TV tenda ya kuonyesha michezo ya Ligi Kuu haikua na usawa, kampuni hiyo bado haijaanza hata matangazo, haijulikani ofisi zake zilipo, uwezo wa kurusha matangazo haujulikani kwa watanzania lakini bado wamepewa nafasi hyo.
Kikubwa tunamuomba rais wa TFF Leodgar Tenga kulitazama suala hili kwa umakini, kwani mtazamo wetu viongozi wa kamati ya Ligi wametazama maslahi yao binafsi bila kuzingatia uwezo wa timu na maliasili watu (wapenzi,washabiki).
Huwezi kuipa mgawo sawa timu ya Yanga na timu nyingine ambazo katika mechi zao binafsi wanatapata washabiki 50 kwenye mchezo, wakati Yanga imeongoza kwa mapato katika msimu mzima wa Ligi Kuu ya Vodacom na wastani wa washabiki 8,000 kwa kila mchezo.
Mwisho Makele amesema wanauamini uongozi uliopo na wapo nao bega kwa bega, tunaomba jamii nzima itambue kuwa Yanga inapigania haki zake na hao wote wanaobeza msimamo wetu basi wajibu hoja kwa hoja na sio kuongea tu pasipo kujibu hoja. 

6 comments:

  1. kinacho nichekesha Simba sc baada ya kuvita zile cheque za simba Tv hili wanaona kama aliwahusu.....hawa watu ni wanafki saana.BIG UP Dar young Africans A.K.A " Nyuma mwiko Daima mbele"

    ReplyDelete
    Replies
    1. teteh kweli mike ni mbulula,hivi kweli washabiki wa tz wabinafsi sana,kwa vile hiyo pesa wanapewa wote ingekuwa yanga mngekuwa wa kwanza,mnaoji vi2 ambavyo avina mantiki,mbona mechi zenu zimeonyeshwa bure na susper sport amkulalamika kwavile kampuni ya nje

      Mdau lamadi simiyu

      Delete
  2. kama hiyo azam TV haijaanza kuonesha na hatujui iko wapi YANGA wanayo sababu ya kuhoji. isije ikawa Richmond katika soka. pili, sikubaliani na hoja ya Mwenyekiti wa Yanga kwamba mashabiki kutoenda uwanjani kutazinyima klabu mapato. ikiwa udhamini utakuwa unatija isitoshe watanzania tunapenda mpira. ikiwa ni mpenzi wa yanga kweli itakuwa vigumu kushindwa kwenda uwanjani kama timu yake inacheza. lIGI YA KENYA inamashabiki wachache sana wanaokwenda uwanjani lakini udhamini wa Supersport umevifanya vilabu kuwa afhadhali kifedha. na sasa ligi inaushindani. yanga wasigomee bali waangalie namna ya kulifanya hili liwe bora zaidi kwa ligi bora na timu bora. Mamea Kanumi. Moro.

    ReplyDelete
    Replies
    1. we ujio makampuni ya azam?ila super sport inazijua,mpira majungu kwa vile azam ni kampuni ya tz

      Nenda shule kwanza,hautokuwa na hoja za kimbulula

      Delete
  3. Bigup sana yanga wajibu hoja zenu ndio cha msingi

    ReplyDelete
  4. Mashabiki wa Yanga na viongozi wote ni wabinafsi

    ReplyDelete