
Charlie Morgan, ambaye aliukalia mpira uliotoka nje wakati Chelsea wakitafuta ushindi wa kuweza kuwapeleka fainali, Hazard alipoenda kuufuata ule mpira dogo akawa bado ameukali ndipo winga huyo wa Mbelgiji alimpopiga teke katika kuujaribu kuuchukua mpira huo. Hazard alitolewa kwa kadi nyekundu kwa kosa hilo. Lakini baadae wawili hao walikutana na kumalizana kistaarabu na mchezaji huyo wa Chelsea alisaini koti alilokuwa amevaa kijana Charlie Morgan muokota mipira.
Sasa ikiwa imepita miezi kadhaa tangu tukio hilo litokee - kijana Charlie ameamua kulipiga mnada koti lake lilosainiwa na Hazard kwenye mtandao wa Ebay - na mapato yatakayopatikana yataenda kusaidia wagonjwa wa kansa.
No comments:
Post a Comment