Search This Blog

Tuesday, June 18, 2013

SUNDERLAND NA SYMBION KUJENGA ACADEMY MBILI ZA SOKA DAR ES SALAAM


CEO wa klabu ya Sunderland, Margaret Byrne, ameusifia ushirikiano na Tanzania kwamba ni hatua kubwa kuendelea mbele.
The Black Cats wameingia mkataba na kampuni ya nishati ya Power kujenga cademy kubwa ya soka nchini, ndani ya jiji la Dar es Salaam.
Raisi Jakaya Kikwete alitembelea makao makuu ya klabu ya Sunderland huko Wearside siku ya jumapili katika kukata rasmi utepe wa kuanza kwa project hiyo.
“Ni siku muhimu kwa klabu na klabu na mji wetu,” Byrne alisema.
“Kutembelewa na mheshimiwa Raisi hapa wakati akiwa UK kuhudhuria mkutano wa viongozi wa G8 ni jambo kubwa kutoka kwake na mawaziri wake. Ni zuri sana kwetu.
Hatua za mwanzo kwa ajili ya Academy zilizinduliwa siku hiyo ya jumapili, kwenye tukio ambalo lilihudhuriwa na mwenyekiti wa Sunderland Ellis Short.
Project hiyo itaisaidia Tanzania katika kukuza soka lake pia kuwapa nafasi kubwa vijana wadogo kabisa kuweza kuendeleza vipaji vyao kwenye academy hiyo. 
Sunderland watajenga majengo pamoja na kutoa makocha wa kufundisha.
“Hatua ya kwanza itatuhusisha sisi kufanya kazi na Symbion Power kujenga academy ya kijamii, tukiruhusu watoto wengi kuja na kufurahia kucheza mchezo wa soka,” Byrne alielezea.
“Hatua ya pili itatuhusisha sisi kufanya kazi na Symbion labda ikiwezekana na taasisi nyingine kujenga kituo cha kisasa cha kufundishia soka.
“Tutoa usaidizi mkubwa wa vifaa vingi tunavyotumia kwenye academy yetu ya Academy of Light na pia na maarifa tuliyoyapata na tunayoyapata kutoka kwenye project ya EPPP (Elite Player Performance Plan).


No comments:

Post a Comment