Search This Blog

Thursday, June 27, 2013

OFFICIAL: ISCO ASAINI MKATABA WA MIAKA 5 KUJIUNGA NA REAL MADRID.

Klabu ya Real Madrid imedhibitisha kumsajili kiungo mshambuliaji Isco kutoka klabu ya Malaga kwa mkataba wa miaka mitano.
Real Madrid imetangaza taarifa hizi kupitia kwenye tovuti yake na kusisitiza kilichobaki sasa ni kufanyiwa vipimo vya afya.
Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 21 alikuwa pia anawaniwa na klabu ya Manchester City inayonolewa kwasasa na kocha wake wa zamani Manuel Pellegrini aliyekuwa Malaga.

No comments:

Post a Comment