Search This Blog

Friday, June 28, 2013

OFFICIAL: GOLIKIPA WA ZAMANI WA SIMBA AJIUNGA NA YANGA KWA MKATABA WA MIAKA MIWILI

Aliyekuwa golikipa wa timu ya Simba, Azam na Mtibwa Deogratius Munishi maarufu kama Dida amejiunga rasmi na klabu bingwa ya Tanzania bara - Dar Young African.
 
Kwa mujibu wa mmoja wa mjumbe wa kamati ya utendaji ya Yanga Abdallah Bin Kleb ni kwamba Dida amesaini mkataba wa kuitumikia Yanga kwa miaka miwili akiwa 'free agent' (mchezaji huru).
 
Dida ambaye alisajiliwa na Azam akitokea Mtibwa na kuweza kujijengea nafasi katika kikosi cha kwanza cha AZAM kabla ya miezi kadhaa iliyopita kusimamishwa na wachezaji wenzie Erasto Nyoni, Said Morad, Aggrey Morris kwa tuhuma za kupokea mlungura na kusababisha timu yao kufungwa na Simba katika mchezo wa raundi ya kwanza wa ligi kuu msimu uliopita.
 

1 comment:

  1. ehe vipi tena yanga mnafanya kama simba ?kusajili golkipa? haya sasa nani ataondoka ?yetu macho.

    ReplyDelete