Search This Blog

Wednesday, June 26, 2013

MKATABA MNONO WA CHELSEA NA ADIDAS WAMPA MOURINHO MSULI WA KUPAMBANA KWENYE SOKO LA USAJILI BILA KUHOFIA 'FINANCIAL FAIR PLAY'

JOSE MOURINHO amewashiwa taa ya kijani ya kuanza kufanya balaa kwenye usajili baada ya Cheslea kusaini mkataba mnono wa £300million na kampuni ya utengenezaji wa mavazi ya kawaida na kimichezo ya adidas.

Mkataba wa miaka 10 baina ya Chelsea na Adidas ndio unaoshika nafasi ya kwanza kwa thamani baina ya klabu na kampuni ya utengenezaji jezi za klabu husika.

Mkataba huo umeondoa wasiwasi wa Chelsea kuvunja sheria za  Financial Fair Play.
Dili hilo la Chelsea na Adidas limevunja rekodi ya dili la Manchester United na Nike lilokuwa na thamani ya  £287m ambalo lilisainiwa miaka 13 iliyopita na linaisha mwaka 2015. 

Mkataba unamaanisha Chelsea hawatokuwa wakimtegemea zaidi Abramovich kuvunja benki katika kuiwezesha timu hiyo.
Mkataba uliopita na Adidas ulisainiwa mwaka 2006 ulikuwa na thamani ya £20million kwa mwaka.

No comments:

Post a Comment