Search This Blog

Saturday, June 1, 2013

MANCHESTER UNITED INAVYOZIZIDI BARCELONA NA REAL MADRID KWENYE KUINGIZA FEDHA NYINGI KWENYE UDHAMINI WA JEZI


Real Madrid, klabu inayoongoza kuwa thamani kubwa zaidi duniani ($3.3 billion), imesaini dili la udhamini wa jezi na kampuni ya Emirates ambao utaiingizia klabu hiyo $39 million kwa mwaka kwa kipindi cha miaka 5.
 
Dili hilo na kampuni ya ndege ya Dubai limeshindwa kuipa Madrid fedha nyingi kama ilivyo kwa vilabu vingine vya juu barani ulaya.
 
Ndio, Los Blancos watapata asilimia 30 zaidi ya walichokuwa wakipewa na mdhamini wa sasa Bwin. Lakini kiasi hicho wanacholipwa na Emirates ni kidogo ukifananisha na wanacholipwa Manchester United(yenye thamani ya $3.2 billion) na Barcelona($2.6 billion) kwenye mikataba yao ya udhamini wa jezi. Mashetani wekundu wameingia mkataba na Chevrolet utakaowaingizia kiasi cha $80 million kwa mwaka kuanzia msimu wa 2014-15 - kwa miaka 5, wakati Barcelona wana mkataba wa miaka mitano Qatar Foundation wenye thamani ya $44 million kwa mwaka - dili linaloanza mwezi ujao.
 
Real Madrid walitakiwa kupewa angalau dili lenye thamani ya kuzidi lile la Barcelona - ikitajwa kuwa klabu yenye mafanikio zaidi kwenye karne hii, imeshinda mataji mengi zaidi ya La Liga na Champions League, pia kwa sasa ina mchezaji mkubwa na maarufu zaidi kwenye ulimwengu wa mitandao ya kijamii Cristiano Ronaldo.

 LISTI YA TIMU ZINAONGOZA KWA KUINGIZA FEDHA NYINGI KUPITIA UDHAMINI WA JEZI



No comments:

Post a Comment