Search This Blog

Thursday, June 20, 2013

KALI YA LEO: MCHEZAJI MPYA WA ASTON VILLA ALALA USINGIZI AKIWA ANAFANYIWA VIPIMO VYA AFYA


Mchezaji mpya wa Aston Villa aliyesajiliwa kwa ada ya £4million Jores Okore alikuwa hana wasiwasi hata kidogo juu ya uhamisho wake kwenda Aston Villa kiasi kwamba wakati akiwa anafanyiwa vipimo vya afya akapitiwa na usingizi kabisa.

Mchezaji huyo mwenye miaka 20 anayetokea FC Nordsjaelland aliweza baadae kuamka na kwenda kusaini mkataba wa miaka minne na Villa. 

Mdenmark huyo, ambaye ameshaichezea timu yake ya taifa mechi 7, alikaririwa akisema: “Nikiwa nafanyiwa vipimo vya MRI scan nilikuwa natakiwa nikae kimya - mawazoni nikawa nafikiria namna maisha ndani ya jiji la Birmingham yatakavyokuwa. Namna nitakavyokuwa naongea kiingereza, lakini hatimaye nikalala baada ya lisaa limoja na nusu kwenye vipimo na nikaamka saa moja baadae."

No comments:

Post a Comment