Search This Blog

Friday, May 3, 2013

KALI YA LEO: MKURUGENZI WA DORTMUND AJIFUNGIA CHOONI KUOGOPA COMEBACK YA REAL MADRID


Mkurugenzi mtendaji wa Borussia Dortmund Hans-Joachim Watzke alikuwa kwenye hali ngumu mno katika dakika z mwish za mchezo wa pili wa nusu fainali ya Ligi ya mabingwa wa ulaya dhidi ya Real Madrid kiasi cha kuacha kuangalia mpira na kukimbilia chooni.

Borussia Dortmund walikuwa wakishambuliwa kama nyuki huku Madrid wakipata mabao mawili ya haraka haraka hivyo kukaribia kuwatoa Wajerumani hao ikiwa wangepata bao lingine.

Mwishoni Dortmund wakakaza na kufanikiwa kuitoa Real kwa jumla ya mabao 4-3, lakini Watzke anakiri dakika za mwisho za mchezo huo zilikuwa ni ngumu kuliko zote katika maisha yake ya uongozi wa soka.


Alisema: “Inaonekana tunapenda sana kujipa presha wenyewe
“Kwa mara kwenye maisha yangu ya soka niliacha kuangalia mpira kwa kuhofia matatizo ya moyo wangu.

Ilinibidi niende chooni kwenye dakika za mwisho, nikajifungia, nikayafunga masikio yangu na nikawa naangalia tu muda kwenye saa yangu.


“Nilikuwa kwenye hali mbaya sana - mawazo kibao yalikuwa ndani ya kichwa changu kwa muda ule.”

Watzke hakuwa kiongozi pekee wa Dortmund aliyekuwa kwenye hali mbaya kiasi cha kutishia afya yake. Mkurugenzi wa michezo wa Borussia Michael Zorc alikiri nae nusra apate mshtuko wa moyo.


No comments:

Post a Comment