Search This Blog

Saturday, May 11, 2013

HATIMAYE WAYNE ROONEY AZUNGUMZIA SUALA LA KUIFUTA MAN UNITED KWENYE UKURASA WAKE WA TWITTER

Siku chache baada ya vyomo vya habari ulimwenguni kuripoti juu ya suala la mchezaji Wayne Rooney kuifuta klabu yake ya Manchester United katika ukurasa wake rasmi wa Twitter, jana usiku mshambuliaji huyo wa England aliamua kujibu mapigo kwa kusema vyombo vya habari vimeandika upumbavu.

Katika taarifa aliyoitoa kupitia mtandao wake binafsi, Ronney alisema: "Kumekuwepo na upumbvu mwingi unaoandikwa kuhusu mimi kubadili biography yangu ya Twitter kwa kuifuta Manchester United kutoka kwenye wasifu huo.
"Sijawahi kuifuta manchester United kutoka kwenye wasifu huo kma magazeit yanavyoripoti kwa sababu sikuwahi kuandika tangu nijiunge na Twitter.
"Kilichotokea ni kwamba niliambiwa na wadhamini wangu Nike kuongeza '@nikeuk' katika wasifu huo kma ilivyo kwa wanamichezo wengine wanaowadhamini.
"Cha kufurahisha hakuna aliyeandika kuhusu hilo! Badiliko hilo lilitokea wiki tatu zilizopita na bado wanaongelea kuhusu kitu hicho kama ni kitu ambacho nimekifanya jana." alimaliza Rooney ambaye anatajwa kwamba ameomba kuondoka Manchester United mwishoni mwa msimu.

No comments:

Post a Comment