Search This Blog

Thursday, May 2, 2013

EXCLUSIVE: HATIMAYE NSA JOB APELEKA JINA LA KIGOGO ALIYEMPA RUSHWA TFF

MSHAMBULIAJI wa Coast Union, Nsa Job amewasilisha barua kwenye Shirikisho la soka (TFF) ambayo inamtaja kigogo ambaye alimpa rushwa.

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), lilimtaka mchezaji huyo kujieleza kutokana na kukaririwa akiongeza katika kituo kimoja cha radio akikiri kupokea rushwa ya sh2mil kwa mmoja wa kiongozi wa timu kubwa ili acheze chini ya kiwango pindi walipokuwa wanacheza na timu hiyo.

Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah, alisema kuwa tayari mchezaji huyo amekwisha tuma barua ya kujieleza nao wameamua kulipeleka suala hilo katika kamati ya nidhamu ambayo inatarajiwa kukutana wiki ijayo.

Alisema mbali na suala hilo pia kamati hiyo itapitia mambo mbali mbali ya ligi kuu ambayo yametokea ikiwemo suala la viongozi ambao walikuwa wanatoa maneno ya uchochozi.

Alisema viongozi wanatakiwa kufuata taratibu na kanuni za soka sio kuongea ongea vitu visivyo na maana ambavyo vitaleta matatizo katika soka.

Moja ya Viongozi ambao watajadiliwa ni Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga baada ya kudaiwa kutoa maneno ya uchochezi pindi TFF, walipohairisha mechi yao dhidi ya Mgambo JKT ya Tanga.  

3 comments:

  1. Huyu ni kaburu hamna mwingine, amezoea haka kamchezo

    ReplyDelete
  2. Sanga kuongea ukweli anajadiliwa! Why wacmjadili Angetile mwenyewe kwa kuwa na jeuri dhidi ya naibu waziri ktk mustakabari mzima wa uchaguzi coz yaleyale ya waziri kuikataa katiba mpya ya TFF ndo hata FIFA wamefanya hivyohivyo? Wafanye kazi siyo kutishiana bhana. Angetile nlikwamini sana ulipokuwa Mwanaspoti na kila wiki nlikuwa msomaji wa makala zako bt now sina iman hata chembe, malizen muda wenu basi.

    ReplyDelete
  3. ni sawa na WAMTAJE SASA WASIFICHE

    ReplyDelete