Search This Blog

Thursday, April 18, 2013

WATANZANIA WASHINDWA KUFANYA VIZURI KIPINDI CHA TANO CHA GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE

 Washindi wa kipindi cha tano cha Guinness Football Challenge Ken Muturi (kushuto) na Chis Mwamgi(kulia) wakishangilia ushindi walioupata huku wakiwa wamebeba pesa taslimu walizojishindia katika shindano hilo jana usiku na pembeni ni mmoja wa watangazaji wa kipindi hicho Lary Asengo(anayepiga makofi kulia).
Washindi wa kipindi cha Tano cha Guinness Football Challenge, Chris Mwamgi(kushoto)  na Ken Muturi(kulia) katika picha ya pamoja na watangazaji wa kipindi hicho Larry Asego and    Flavia Tumsiime jana baada ya ushindi.


 Jana usiku kupitia Televisheni za ITV na Clouds TV timu ya Tanzania ilishindwa kutumia nafasi ya kipindi cha mwisho cha mashindano ya “Guinness Football Challenge” katika hatua ya Afrika Mashariki baada ya kutolewa na timu kutoka Kenya. Rangi nyekundu imeonekana kuwa ni rangi ya bahati kwa timu za Kenya kwani hii ni timu ya nne kutoka Kenya kufanikiwa kufuzu kuingia hatua ya Pan-African GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGETM. Kenneth Mukuri na Chris Mwamgi ndio walioibuka washindi jana usiku kwani walifanikiwa kufika katika hatua ya mwisho ya kulenga ukuta  wa pesa wa Guinness ambapo walijishindia dola za kimarekani  1,500.

Ni vipi Kenneth na Chris wataweza kumudu hatua ya Pan-African? Sasa wana nafasi ya kuiwakilisha nchi yao katika mashindano ya Pan-African ambapo watakutana na wawakilishi pekee kutoka Tanzania, Daniel Msekwa na Mwalimu, washiriki kutoka Uganda Alex Muyobo na Ibrahim Kawoova pamoja na wenzao kutoka Kenya,Francis Ngigi na Kepha Kimani(washindi wa kipindi cha 2), Kenneth Kamau na Wills Ogutu(washindi kipindi cha 3) na Ephantus Nyambura na Samuel Papa(washindi kipindi cha 4).

Timu hizi tano zitakua uwanjani kutimiza malengo yao, ambapo watakutana uso kwa uso na washiriki kutoka Ghana na Cameroun kuonesha ni nani ana maarifa zaidi na ujuzi wa kusakata kabumbu,  hata kuvishwa ubingwa wa Pan-African na  kuondoka na dola za kimarekani 250,000.

Usikose kuangalia mashindano haya kupitia televisheni za ITV na Clouds TV huku ukiburudika na kinywaji cha GUINNESS.
                                                                                                                                         
Tafadhali kunywa kistaarabu - Hairuhusiwi kwa wenye umri chini ya miaka 18.

No comments:

Post a Comment