Search This Blog

Thursday, April 11, 2013

JAY Z KUUZA HISA ZAKE BROOKLYN NETS ILI KUWA WAKALA WA WACHEZAJI WA NBA - NETS KUPOTEZA JINA KUBWA KWENYE BIASHARA


Mwanamuziki nguli na tajiri yupo katika hatua za mwisho za kuuza hisa zake kwenye timu ya mpira wa kikapu ya Brooklyn Nets ili aweze kuwa wakala wa wachezaji wa NBA, ikiwezekana kabla ya mwisho wa msimu. Mpango huo kwa sasa upo katika kuufanikisha, mtu mmoja mwenye ukaribu wa kambi ya Jay Z alisema jana Jumatano.
Sheria za NBA zinakataza mtu yoyote mwenye miliki kwenye timu kufanya kazi ya uwakala kwa wachezaji.
Hivi karibuni Jay Z kupitia kampuni take ya Roc Nation aliingia mkataba wa ushirikiano na Creative Artists Agency (CAA) na matumaini yao ni kuanza kushindani dili za kuwakilisha wachezaji wa NBA kuanzia mwezi June mwaka huu.   
Jay-Z anamiliki asilimia chache sans kwenye timu ya Nets, lakini amesaidia sans katika kuitangaza timu hiyo na kuihamisha kutoka New Jersey kwenda Brooklyn. Alikuwa mstari wa mbele katika kukamilisha makao makuu ya timu hiyo yenye thamani ya $1 billion ya Barclays Center, pia akisaidia katika ubunifu wa jezi mpya za timu hiyo. Kisha akaizindua Barclays Center kwa shows nane mfululizo kwa mafanikio kwa kuuza tiketi zote. 
Jay Z ambaye ni mume wa mwanamuziki Beyonce ana urafiki na wachezaji wengi wakubwa wa NBA, Lebron James na winging kibao, kwa haraka Jay Z anaweza kufanikiwa sans kwenye biashara hiyo ya uwakala. 
Jay Z na kampuni yake mpya ya uwakala hivi karibuni alimsaini  star wa New York Yankees All-Star Robinson Cano. 

No comments:

Post a Comment