Search This Blog

Wednesday, April 24, 2013

ADHABU ALIYOPEWA SUAREZ YA KUFUNGIWA MECHI 10 UKILINGANISHA NA ADHABU ZA MATUKIO MENGINE YALIYOFANYWA NA WACHEZAJI WENGINE NCHINI ENGLAND


 Muda mchache uliopita Chama cha soka cha England kimetangaza kufungiwa kwa mchezaji Luis Suarez kwa mechi 10 kwa kosa la kumng'ata Branslav Ivanovic katika mchezo wa ligi kuu ya England wiki iliyopita.

Huko nyuma kumekuwepo na matukio ya vurugu uwanjani yaliyofanywa na wachezaji na adhabu zake zikaishia katika kufungiwa mechi kadhaa - sasa tujaribu kuangalia matukio hayo na adhabu zilizotolewa na kufananisha na hii ya sasa Suarez

ADHABU YA MECHI 12

Duncan Ferguson (Rangers): Mchezaji huyu alipewa adhabu ya kufungiwa mechi 12 kwa kumpiga kichwa mchezaji wa Raith aitwaye John McStay mnamo mwaka 1994

Joey Barton (QPR): Mtukutu Joey Barton nae yupo katika nafasi ya kwanza kwa kufungiwa mechi 12 kwa kumpiga kichwa mchezaji wa Manchester City katika mechi ya mwisho ya ligi kuu msimu uliopita.

 

MECHI 11

Paolo Di Canio (Sheffield Wednesday): Kocha wa sasa wa Sunderland ni mmoja kati ya wachezaji watukutu ambao wameshawahi kucheza kwenye ligi kuu ya England - mnamo mwaka 1998 alimsukuma refa Paul Alcock na kwa kitendo hicho akafungiwa mechi 11.

MECHI 10 

Kevin Keegan (Liverpool) na Billy Bremner (Leeds): hawa magwiji wa soka walifungiwa mechi 10 kwa kitendo chao cha kupigana katika mechi ya kombe la hisani mwaka 1974
David Putton (Southampton): Kama ilivyokuwa kwa Di Canio - Alan Wiley nae alimsukuma refa mwaka 2005 na akafungiwa mechi 10.

NINE MATCHES

Paul Davis (Arsenal): Alifanya kosa la kumpiga ngumi Glenn Cockerill mwaka 1998.
Steve Walsh (Leicester) kwa utovu wa nidhamu mnamo mwaka 1987
Frank Sinclair (West Brom): Kwa kitendo cha kujaribu kumpiga kichwa refa mnamo mwaka 1992

EIGHT MATCHES

Luis Suarez (Liverpool): Kwa kumtolea matusi ya kibaguzi mchezaji wa Manchester United Patrice Evra mnamo mwaka  2011
Ben Thatcher (Manchester City): Kwa kosa la kumpiga kiwiko Pedro Mendes mwaka 2006
Mark Dennis (QPR): Alifungiwa mwaka 1987 kwa kupata kadi nyekundu ya 11 ndani ya ligi kuu ya England.

No comments:

Post a Comment