Search This Blog

Thursday, March 7, 2013

YANGA VS TOTO: BARTHEZ HALI TETE ASHINDWA KUFANYA MAZOEZI NA YANGA

KIPA wa Yanga, Ally Mustapha 'Barthez' ameshindwa kufanya mazoezi na wenzake leo kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya tumbo. 

Yanga inajiwinda na mchezo wake wa ligi dhidi ya Toto African ya Mwanza utakaopigwa Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Daktari wa Yanga, Nassor Matuzya alisema jana asubuhi, baada ya mazoezi ya timu hiyo, Uwanja wa Bora Kijitonyama, Dar es Salaam;
 

"Barthez ameshindwa kufanya mazoezi na wenzake leo kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya tumbo." Matuzya alisema; "Vipimo vimeonyesha chakula alichokula juzi usiku ndicho kimemsababishia hali hiyo.

"Kwa sasa hali yake inaendelea vizuri. Natarajia kesho atajiunga na wenzake kuanza mazoezi."
 

Hata hivyo, daktari huyo alisema hawezi kuweka wazi kuwa atakuwepo katika mchezo wa Jumamosi. "Siwezi kuweka asilimia 100 kuwa Barthez atakuwa fiti kucheza dhidi ya Toto. Nafikiri tusubiri hiyo kesho."
 

Pia, beki wa kulia Juma Abdul na kiungo Nurdin Bakari walishindwa kufanya mazoezi na wenzao kutokana na kuwa majeruhi.
 

"Nurdin anasumbuliwa na goti kama ilivyo kwa Abdul. Kwa sasa hali zao zinaendelea vizuri. Lakini nafikiri kuanzia kesho watajiunga na wenzao kuanza mazoezi."

No comments:

Post a Comment