Search This Blog

Tuesday, March 5, 2013

PETER CECH AMTETEA ABRAMOVICH - AWAULIZA ARSENAL KAMA WANGEKUWA TAYARI KUFUNDISHWA NA MAKOCHA 10 NA KUSHINDA MAKOMBE?

Huku kukiwa na hatari ya kupoteza ajira kwa kocha Rafael Benitez kwenye klabu ya Chelsea, golikipa Peter Cech ameamua kuweka mtazamo wake kwenye mlengo chanya kuhusu mmiliki wa klabu hiyo Roman Abramovich na tabia yake ya kutokuwa mvumilivu na makocha pindi timu inapofanya vibaya. 

Akizungumza na The Guardian alisema: 
"Unaweza ukazungumza mengi kuhusiana na hili suala, lakini pia katika kipindi hicho hicho tumeshinda kama au pungufu ya Manchester United," alisema. "United wamekuwa na kocha mmoja, sie tumekuwa nao nane, na tumeshinda makombe sawa, wameshinda champions league hata sie tumeshinda. Kuna vitu vingi chanya tumepata
          "Arsenal wamekuwa na kocha mmoja na ni muda mrefu hawajashinda hata kikombe    kimoja. Labda uwaulize wenyewe kama wangekuwa radhi kuwa na makocha 10 na makombe sita, sijui wangejibu nini lakini nadhani kila klabu ina namna yake ya kufanya kazi zake."


No comments:

Post a Comment