Search This Blog

Saturday, March 16, 2013

LIVE MATCH CENTRE: YANGA SC 1 - 0 RUVU SHOOTING FULL TIME

Dk 90 FULL TIME! YANGA 1-0 RUVU

Dk 83 Ruvu imefanya mabadiliko, ametoka Ayoub Kitala ameingia Raphael Kyala.

Dk 80 Yanga imefanya mabadiliko, ametoka Nizar ameingia Didier Kavumbagu.

Dk 78 Mangasini wa Ruvu anamchezea vibaya Nizar wakati akiwa katika harakati za kufunga. Nizar hawezi kuendelea na mchezo.

Dakika ya 75, Ruvu Shooting 0 - 1 Young AfricansDk 72 Yanga inatawala mchezo kwa kucheza mpira wa pasi nyingi.

Dakika ya 60, Ruvu Shooting 0 - 1 Young Africans

Dk 56 Ruvu wanafanya mabadiliko, ametoka Gideon Tepo ameingia Paul Ndauka.

Dk 55 Kiiza anashindwa kuunga kwa kichwa krosi ya Nizar.

Dk 50 Mangasini Mangasini wa Ruvu anampiga kiwiko Domayo lakini mwamuzi hajaona.

Wakati wa mapumziko Yanga ilifanya mabadiliko, ametoka Joshua ameingia David Luhende.

Dakika ya 48, Hamis Kiiza anaipatia Young Africans bao la kwanza
Ruvu Shooting 0 - 1 Young Africa

Kipindi cha pili cha mchezo kimeanza, Ruvu Shooting 0 - 0 Young Africans

Dk 45 HALF TIME! YANGA 0-0 RUVU.

Dk 43 Nizar wa Yanga anayecheza kama straika leo, anaonekana amechoka na kushindwa kuziwahi pasi na krosi nyingi zinazopigwa eneo lake.

Dk 39 Kipa wa Ruvu, Benjamin Haule anadaka kwa ustadi krosi ya Msuva huku Nizar akiwa tayari kuiunganisha.

Dk 36 Beki wa Yanga, Oscar Joshua anaonyeshwa kadi ya njano na mwamuzi Jacob Adongo baada ya kumchezea rafu Said Dilunga.

Dakika ya 30, Ruvu Shooting 0 - 0 Young Africans

Dk 28 Said Dilunga wa Ruvu anakosa bao la wazi akiwa amebaki na kipa wa Yanga.

Dk 25 Ruvu wanapata kona baada ya Cannavaro kuutoa mpira nje. Kona isiyo na madhara imepigwa.
Dk 23 Mbuyu Twite wa Yanga anachezewa faulo na Said Dilunga.

Dk 22 Cannavaro anamchezea rafu Said Dilunga wa Ruvu.

Dk 19 Yanga imeongeza mashambulizi langoni kwa Ruvu. YANGA 0-0 RUVU.

DK 15, Ruvu Shooting 0-0 Yanga

Dk 10 Beki wa Yanga, Nadir Haroub 'Cannavaro' amemchezea faulo Abrahman Musa wa Ruvu. Timu zinashambuliana kwa zamu.

Dk 8 Kipa wa Yanga, Ally Mustapha 'Barthez' anapangua shuti kali la Michael Aidan wa Ruvu lililopigwa kutoka nje ya eneo la hatari.

Dk 7 Frank Domayo wa Yanga anachezewa faulo na Ayoub Kitala wa Ruvu.

Dk 4 Hamis Kiiza wa Yanga anapiga shuti kali langoni kwa Ruvu akiunganisha pasi ya Nizar Khalfani lakini kipa Benjamin Haule anaudaka mpira.

Mpira ndio umeanza hapa Uwanja wa Taifa kati ya Ruvu Shooting Vs Young Africans

Wachezaji wa timu zote na watazamaji wamesimama kwa dakika moja kuomboleza kifo cha kocha na mchezaji wa zamani wa Pan African marehemu mzee Athuman Chilambo.

Young Africans line-up to face Ruvu Shooting today:
1.Ally Mustafa 'Barthez'
2.Juma Abdul
3.Oscar Joshua
4.Nadir Haroub 'Cannavaro'
5.Mbuyu Twite
6.Athumani Idd 'Chuji'
7.Saimon Msuva
8.Frank Domayo
9.Nizar Khalfani
10.Hamis Kiiza
11.Haruna Niyonzima

Subs:
1.Said Mohamed
2.Shadrack Nsajigwa
3.David Luhende
4.Nurdin Bakari
5.Said Bahanuzi
6.Jerson Tegete
7.Didier Kavumbagu

RUVU SHOOTING: Benjamin Haule, Michael Aidan, Mau Bofu, Ibrahim Shaban, Mangasini Mangasini, Gideon Tepo, Ayoub Kitala, Ernest Ernest, Hassan Dilunga, Said Dilunga, Abrahman Musa

No comments:

Post a Comment