Search This Blog

Wednesday, March 6, 2013

CRISTIANO RONALDO ANAWEZA AMERICAN FOOTBALL - AKIRI REGGIE BUSH

Katika kusherehekea kutimiza miaka 28 ya kuzaliwa kwake siku ya jumamosi iliyopita, mchezaji wa timu ya mchezo american football Red Bull Reggie Bush alipewa ofa ya kwenda kuangalia El classico nchini Spain kati ya Real Madrid na Barcelona.

Real Madrid wakashinda 2-1 kwenye uwanja wao wa nyumbani Santiago Bernebeu, lakini walishindwa kumzuia Messi asifunge goli ake la 39 kwenye La Liga. Raggie Bush anakiri alishangazwa na uwezo wa mchezaji huyo kiargentina namna anavyofanya uone mchezo wa soka ni rahisi.

Lakini alipoulizwa na mchezaji gani kwenye el classico anaweza kwenda kucheza kwenye American Football, Reggie alisema bila shaka ni Cristiano Ronaldo, "Ni kweli Ronaldo anaweza kucheza NFL, Ni mrefu wa kimo 6'1", 6'2", na anakimbia sana. Itakuwa jambo la kuvutia kumuona Ronaldo akipambana kwenye NFL, paia mie kama ningepata nafasi ya kucheza soka ningependa kuwa Ronaldo na kucheza nafasi ya ushambuliaji."

Reggie Bush na Cristiano Ronaldo wana historia ya kuvutia kidogo pamoja, wote wamewahi kuwa na mahusiano na mwanadada Kim Kardashian.

No comments:

Post a Comment