Search This Blog

Wednesday, March 13, 2013

BARCELONA NA TIMU NYINGINE ZILIZOWEZA KUENDELEA MBELE KWENYE HATUA YA MTOANO BAADA YA KUPOTEZA MECHI YA KWANZA KWENYE CHAMPIONS LEAGUE


Kwa ushindi wao 4-0 victory katika hatua ya 16 bora dhidi ya AC Milan, FC Barcelona imekuwa timu ya tano kwenye historia ya Champions League kushinda kwenye hatua ya mtoano baada ya kufungwa kwenye mechiya kwanza kwa bao 2 au zaidi - na timu ya kwanza kufanya hivyo bila kunufaika na goli la ugenini. Hizi ni timu nyingine zilizowahi kupata matokeo mazuri baada ya kufungwa kwenye mechi ya kwanza.

 
AC Milan 4-1 RC Deportivo La Coruña
RC Deportivo La Coruña 4-0 AC Milan
2003/04 robo fainali
Walter Pandiani aliipa uongozi Deportivo San Siro, lakini mambo yalibadilika mpaka kufikia full time, huku Kaká akifunga mara mbili na kuikata maini Deprtivo. Kuelekea kwenye mechi ya marudiano kwenye dimba la Riazor, kocha wa Deportivo Javier Irureta alikuwa hana matumaini yoyote zaidi ya ndoto.
Lakini kwa maajabu, mpaka kufikia mapumziko kikosi cha Depor kilikuwa mbelel kwa aggregate, Pandiani, Juan Carlos Valerón na Alberto Luque waliipa uongozi wa 3-0, baadae mchezaji aliyetokea benchi Fran González aliongeza goli la nne dk 76 na mwishowe wakapita kuingia nusu fainali. 

 
Real Madrid CF 4-2 AS Monaco FC
AS Monaco FC 3-1 Real Madrid CF
2003/04 robo fainali
Matumaini yoyote yaliyokuwepo kwa Monaco kwenda nusu fainali yalipotea baada ya filimbi ya mwisho kupulizwa pale Santiago Bernabeu tarehe 24 March 2004. Mabao manne ya Madrid mpaka kufikia half time yalishawakatisha tamaa, lakini bao la dakika 83 kutoka Fernando Morientes kwa Monaco lilileta matumaini. Kocha Didier Deschamps akagoma kukubali kutolewa mapema. 

Kwenye mechi ya pili wakatanguliwa lakini Ludovic Giuly akasawazisha, Morientes akiwa Monaco kutoka mkopo Madrid akaongeza la pili na Giuly akapiga la tatu na kufanya matokeo yawe 3-1. Hatimaye magoli ya ugenini yakaipitisha Monaco kwenda nusus fainali. 


Chelsea FC 3-1 FC Barcelona
FC Barcelona 5-1 Chelsea FC (aet)
1999/2000 robo fainali
Kabla ya utawala wa Roman Abramovich, Chelsea hawakuwa na nguvu kama waliyonayo hivi sasa, na ushindi wao wa kwenye mechi ya kwanza robo fainali dhidi ya kikosi cha Louis van Gaal cha Barcelona – mabao ya Gianfranco Zola na mawili ndani ya dakika nne ya Tore André Flo yakiwapa kifua mbele vijana wa  Gianluca Vialli. Mechi ya pili kibao kikawageukia watoto wa darajani, Barcelona iliyoundwa na akina Rivaldo, Figo, Kluveirt na wenzao wakiwa mbelel ya mashabiki wao 90,000 wakaiadhibu Chelsea 5-1 kwenye ulioenda mpaka extra time.

 
SSC Napoli 3-1 Chelsea FC
Chelsea FC 4-1 SSC Napoli (aet)
2011/12 hatua ya 16 bora
Hii ndio mechi ya mwisho kwa Andre Villas Boas kwenye champions league ambapo Chelsea walishushiwa kipigo cha mabao 3-1 mjini Naples; Juan Mata alifunga bao muhimu baada ya Ezequiel Lavezzi kufunga mara mbili na Edinson Cavan kupiga moja, wakimuacha Villas Boas akisema kwamba bao la ugenini linaweza likawapa nafasi ya kusonga mbele kwenye mchezo wa marudiano.  

Kwa bahati mbaya, Mreno huyo hakupata bahati ya kuiongoza Chelsea kwenye mechi ya marudiano alitimuliwa nafasi yake ikachukuliwa na Roberto Di Matteo kwenye mchezo huo ambao Didier Drogba, John Terry and Frank Lampard waliibeba Chelsea kusonga mbelel katika mechi iliyoenda mpaka kwenye muda wa ziada.

No comments:

Post a Comment