Search This Blog

Thursday, January 10, 2013

MACHANGUDOA NCHINI BRAZIL WAANZA KUJIFUNZA KIINGEREZA KWA AJILI YA KOMBE LA DUNIA NA MABARA

Christ the Redeemer
 
 
Machangudoa katika moja ya miji mikubwa nchini Brazil wameanza kujiunga na madarasa yanayotoa elimu ya bure ya lugha ya kiingereza kuelekea kwenye michuano ya kombe la mabara na 2014 World Cup. 

Cida Vieira, raisi wa chama cha machangudoa katika jiji la Belo Horizonte, alisema juzi Jumanne kwamba machangudoa 20 tayari walishajiunga na kozi hiyo na anategemea wengine kama 300 katika kundi la wanachama 4,000 kuwafuata wenzao. 

Chama cha hicho kimeandaa madarasa na sasa wanatafuta waalimu. 

"Sidhani kama tutapata matatizo ya kuwapata waalim wa kiingereza kutoa elimu ya bure," alisema. "Tayari tumeshapata wanasaikolojia na madaktari watakaotoa huduma bure." 

Amesema madarasa yataanza kutoa elimu kuanzia mwezi March na yatadumu kwa muda wa miezi nane. 

"Litakuwa jambo muhimu kwa wasichana ambao wataweza kutumia lugha ya kiingereza ili kuzungumza na wateja wao na kukubaliana bei na vitu vingine." aliongea Cida kupitia simu. 

"Pia kwa sababu hiyo hiyo tutakuwa tunatoa elimu ya lugha ya kifaransa na kiitaliano." aliongeza.

Biashara ya kujiuuza ni halali huko nchini Brazil. 

Uwanja Mineiro uliopo kwenye mji wa Belo Horizonte
unachukua watazamaji 62,000, na utatumika kuchezewa mechi tatu kwenye kombe la mabara na mechi 6 kwenye kombe la dunia.

No comments:

Post a Comment