Search This Blog

Thursday, January 10, 2013

GARETH BALE AMTAJA RONALDO KUWA MCHEZAJI BORA WA DUNIA ALIYEKAMILIKA - HUKU AKITUPIA HAT TRICK SIKU MOJA BAADA YA KUKOSA BALLON D'OR


sSiku moja baada ya kupotezwa vibaya na Lionel Messi katika tuzo za mchezaji bora wa dunia, Cristiano Ronaldo anaonekana amerudi kiwanjani kuja kuthibitisha uwezo wake kwa vitendo baada ya jana usiku kurudi dimbani na kutupia hat trick katika mechi ya pili ya kombe la mfalme dhidi ya Celta Vigo.

Katika mchezo huo wa jana Madrid walishinda kwa jumla 4-0, Khedira akifunga 1 na Cristiano akitupia matatu, hivyo kusonga mbele kwa jumla ya mabao 5-2.

Wakati Ronaldo akitupia hat trick hiyo, mchezaji wa Tottenham Hotspur Gareth Bale aliandika kwenye mtandao wa Twitter kwamba anaamini Cristiano Ronaldo ndio mchezaji bora wa dunia aliyekamilika huku akisema Ronaldinho na Cristiano Ronaldo ndio wachezaji bora kabisa aliowahi kucheza dhidi yao.

 

No comments:

Post a Comment