Search This Blog

Wednesday, December 12, 2012

VIPIMO VYA AFYA, BANGI, UTOTO NA MAPENZI YA YANGA - MAONI YA WASHABIKI KUHUSU SAKATA LA YANGA






21 comments:

  1. Vipimo vya HIV-AIDS ndivyo vilivyomfanya kijana ajifiche! Acha mchezo na kile kipimo!

    ReplyDelete
  2. Akili za Ngasa Zinamtosha Kabisa. Tatizo la hizi timu zetu wanamuuza Ngasa utafikili Gunia la Mahindi. Hajashilikishwa anasikia tu kwenye vyombo vya habari kushusu yeye kauzwa El Meleik, Kama ni wewe ungeenda kisa pesa. Ubinadamu kwanza tusije tukawa watumwa wa pesa

    ReplyDelete
    Replies
    1. hivi wewe unasema alikuwa anauzwa kama gunia la karanga, hujui kuwa yeye ndo alikuwa wa kwanza kuongea na el-mereikh kabla ya azam. Au unaongea tu kishabiki. Dogo ni Kilaza. Akibaki hapa hataendelea kimaisha wala kipesa. Anaacha timu kubwa na hela nyingi. Ndo nyie kesho na keshokutwa mnaanza kusema mpira bongo haundelei

      Delete
    2. Mpira wa bongo haundelei kwa ngassa kukubali kucheza sudan.bali kwa bongo kutokuwa na misingi bora ya mipango endelevu kwenye soka.hao viongozi walikuwa wanawaza kupata pesa tu kwa mgongo wa ngassa deal imekula kwao safari hii.

      Delete
  3. awe na akili ndogo, awe ana elimu ndogo, awe mjinga, awe mtoto, awe na mademu, awe na bangi, awe vyovyote vile mnavyotaka.. ana haki ya kufanya uamuzi wowote ule anaoutaka juu ya maisha yake, hakuna mtu kati ya hawa wanaomlaumu angemjua kama asingekuwa anacheza mpira, je kati ya hawa kuna aliyemshauri acheze mpira. mimi naamini kila binadamu(18+) ana haki ya kuamua mustakabali wa maisha yake..why can't you leave him alone. Ngasa Ngasa kwa nini msiwashauri ndg zenu waende wapi mnaangaika na Ngasa. tujenge utamaduni wa kuheshimu maamuzi ya mtu especially kwa issue ya maisha yake. Ivi Ngasa alipewa nafasi ya kucomment juu ya kazi yako na mahali ulipo ajiriwa....achani tabia ya kudharau watu na kujiona nyie mna akili sana kuliko wengine

    ReplyDelete
  4. mi bado siamini kama kweli Ngassa amejificha ili arudi yanga. kama ni kweli, kwakwel ntamdharau sana!!!...hapo hamna cha mipango stahiki, mi nadhani malengo ya mchezaji inatakiwa kwenda mbele tu na hata aje kuchezea timu kubwa ulaya. sasa kwa mtaji huu, Ngassa anafikiria kweli kuja kucheza hata uefa champions League au walau Carling Cup kweli??...sidhani.!!atakuwa bwege la mwisho kama kweli.

    ReplyDelete
  5. ISSUE SIO KUUZWA ILA NI JINSI GANI ANAWEZA KUJIJUA HUYU, KWANI HAKUNA MTU ANAYE MLAZIMISHA KWENDA SUDANI NA SI RAZIMA ILA ALITAKIWA KUWA MTU ALIYEPEVUKA NA MWEREDI NA KUJIBU SIMU NA SIKUZIMA NA KUTOPOKEA HUO NI UHUNI YEYE SIO MWEZI MPAKA AOGOPE KUPOKEA SIMU. BANGI TU HAKUNA KINGINE, KWANI KESHO TU UTAMSIKIA MIMI NAANGALIA MASLAHI TIMU YOYOTE NACHEZA

    ReplyDelete
  6. hakuna cha uamuzi wake huo ni ujinga na ulimbukeni, anatakiwa akacheze soka sehem nyingine ili ajifunze vitu vingine na apate chalange nyingi tofautitofauti kutoka kwa wenzetu, yy amekomaa kucheza ndondo la bongo, cku hizi watu wanaangalia maslahi kwanza na sio upenzi, unaleta mapenzi ya mpira bongo? viongozi wababaishaji hakuna la maana wanalofanya kukuza soka la bongo kazi kukomoana tuu simba na yanga, then ngasa anajiona bonge la super star kucheza soka la bongo, ujinga huo haigi hata kwa wachezaji wa ulaya? hamuoni drogba kaenda china kwa ajili ya maslahi? ngoja achuje ndio atajutia hizi chance za kumake money, aanze kugongea jero la sigara bwege!! na viongozi wa kibongo ukichuja tuu hawana tena time na ww.... atajuta huyo baadae..

    ReplyDelete
  7. kila mtu ana uamuzi wake ndio maana wapo hadi wanaoamua kuoana kwa jinsia moja na bado wanadai haki yake.kwa wengine haingii akilini kwao inaingia.hata kwa Angasa kwenu haiingii akilini kwake iko akilini.aachiwe uhuru wake.

    ReplyDelete
    Replies
    1. acha kutetea ujinga. Kutopokea simu wakati unajua kuhusu mazungumzo na ulikubali ni uhuni na utoto na ujinga. Angepokea awaambie kama mwanaume kuwa hataki kwenda sudan

      Delete
  8. Utamdharau wewe ni nani? acha ww yaani umaskini wako unataka Ngasa ndo aende Sudani? nenda wewe.

    Pia watu wanashindwa kuelewa ushirikishwaji alikuwa anautaka Ngasa, Ngasa aliwaruhusu Wasudani waongee na kilabu yake sio kwamba ndo tayari alishazungumza nao, kwa mkataba uliobaki miezi 5 Simba na Azam walitakiwa wamshirikishe katika mazungumzo yao sio kukaa wenyewe pekee yao. Pia hivi ule mshahara wa usd4,000/= na ile usd75,000/ nani alinegotiate nao hao wasudani? Ni Ngasa mwenyewe au Simba na Azam ndo waliongea nao kwa niaba ya Ngasa?

    Katika soka letu matatizo ni mengi sana sio wachezaji pekee wenye matatizo hata vilabu vinasababisha haya yote, havina mipango endelevu, Utamuuzaje mchezaji anaemaliza mkataba bila ya yeye kulizia? Haki iko wapi hapo hivyo vitu Ulaya hakuna ndo maana hata RVP alipokaribia kumaliza mkataba Arsenal alikataa kabisa kusaini mkataba mpya hivyo alikuwa anatafuta dili zuri ambalo hata yeye atafaidika ndo akaenda UTD otherwise hata Arsenal ingekula kwao. wewe angalia ni wachezaji wangapi kutoka Amerika ya kusini wanakataa dili la timu za uingereza ambazo zinatoa mshahara mzuri? tatizo sio mshahara tu hata maisha nchi unayoenda, kuna kodi, living cost nk nk. ila kwa upeo wetu sisi tunaona usd 4,000 ndo kaula, hebu kata kodi hapo toa living cost then niambie, ni bora ulipate net ya Tshs. 1m hapa Bongo.

    Kuhusu issue ya Ngasa ni ngumu kujua tatizo ni nn, ila nahisi kile kitendo cha Azam kumpeleka Simba kwa mkopo hakikumfurahisha mchezaji wa kiwango kama cha Ngasa hapa TZ, pia kulikuwa na mizengwe mingi tu mara ana mapenzi na Yanga mara hataki kucheza vizuri akicheza na Yanga. hayo yote na uroho wa pesa wa viongozi wetu ndo uliosababisha Ngasa kukataa dili.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Alikuwa anaitwa ili ashirikishwe, na hata angefika pale asingeshikiwa bastola ili asaini, angesaini kwa ridhaa yake. Sasa kama tatizo ni hela au kitu kingine, utakisema vipi kama hata simu hupokei au unazima. Acha kutetea ujinga.

      Delete
    2. wewe ndiyo unaongea ujinga sioni haja ya ngassa kupokea simu kwa watu wapumbavu wasioelewa hata contract Act haiwezekani umuuze mtu bila hata main product to the contract haijashilikishwa.Acheni kuclaim nyie wajinga kama Azam is always right nao ni malimbukeni tu wasiojua sheria za mikataba wakae kushoto binadamu si mbuzi bwana.

      Delete
  9. nafikiri tutafute kwanza chanzo cha yeye kugoma kwenda kabla ya kumpa lawama maana hiyari ya kwenda au kutokwenda anayo yeye, hata alipopelekwa Simba mwanzoni aligoma kisha akasema yeye ni mpenz wa simba tangu utoto ajabu leo anitaka Yanga tena

    ReplyDelete
    Replies
    1. Lawama za kutopokea simu na kuwazimia simu watu ambao walishakubaliana wataongea hawezi kuzikwepa. Ni utoto na ujinga. Kama mwanaume angepokea simu akubaliane nao au apingane nao, anogopa nini??

      Delete
  10. Huyo ni wa hapa hapa mwacheni kashikiwa akili na wanjanja wa mujini ambao wanaendelea kupata sifa na biashara zao zinakuwa kwa kutumia siasa za mpira wa kibongo. Nina uhakika wa 100% leo hii akienda Kitenge au Sahfii Dauda au mwandishi yeyote wa habari kumuuliza Ngasa nini malengo yako ya baadaye kisoka atajibu bila aibu wala kupepesa macho lengo langu ni kwenda kucheza ulaya! Ajabu ya mwaka kwenda ulaya kirahisi rahisa angalia ramani aliyopita Nonda kufika ulaya na kuwaacha wakina Lunyamila na Bakari Malima wakiwa veterani mapema wakati huo bado Nonda alikuwa anavuna mapesa na walicheza pamoja. Henry Joseph, Samata, Ulimwengu na Nditi wa Chelsea watacheza mpira wa ushindani zaidi ya miaka 10 ijayo ila Ngasa tutacheza naye bonanza leaders miaka 3 ijayo mwenzake Tegete kwa ujinga huo huo si ajabu akaja kwenye bonanza mwakani. No wonder wachezaji veterani Tanzania unakuta wana miaka 27 wakati ulaya ndio wanakuwa kwenye peak.

    ReplyDelete
  11. SAKATA LA NGASA, EL MERREIKH, AZAM NA SIMBA

    Tukumbuke mambo 7 muhimu:
    1. Ngasa kabakiza miezi 5 kumaliza mkataba wake awe huru na baada ya hapo timu ikimtaka anaweza kuchukua pesa zote mwenyewe.
    2. Azam iliamua kumuuza bila yeye na Simba kujua - ushahidi ni kauli ya Zacharia Hans Pope kuwa "eti walijitahidi kumsemea Ngasa na El Merreikh wakaongeza signing fee kutoka dola 30,000 hadi dola 75,000"

    3. Simba ilimchukua kwa mkopo wa lazima toka Azam na wala si mali yao kumwamria kwa kwenda na kudai "share" ambayo Ngasa hapati kama shukrani ya kuwafanyia biashara. Tukumbuke vilabu vinayouza pia huwapa wachezaji sehemu ya mapato ya kuwauza.
    4. Azam ilimrushia vyake na kusema aende kwa mkopo au akae becnhi hadi mkataba wake uishe (tena alihukumiwa bila mashauri yoyote baada ya yeye kuibusu na kuivaa jezi ya Yanga)
    5. Yanga, Simba, Azam nk nao ni muhimu kujiimarisha kwa kuwa na wachezaji bora ili kuhimili vishindo vya mechi za kimataifa na kufikia viwango vya TP Mazembe, Al-Ahly, Kaizaer Chiefs, Esperence, etc.
    6. Tresor Mputu wa TP Mazembe alikataa mara kadhaa kujiunga na Arsenal na Glasgow Celtic na kuamua kubaki Mazembe ili kuifanya Mazembe klabu kubwa Afrika kulingana na vision ya klabu na mmiliki Moise Katumbi.
    7. Vilabu vyetu vijifunze kuwa na ambition ya kuwa bora zaidi Afrika na dunia hivyo kuwa na mikakati sahihi ya kujijenga ikiwa ni pamoja na kubakiza mastaa wako (akina Kapombe, Niyonzima, nk) na kuwaleta wengine ili kutogeuka ni Academies tu kama ambavyo Arsenal wanahangaika sasa.

    Nawasilisha!!!

    ReplyDelete
    Replies
    1. Amwulize Tegete aliedanganywa arudi bongo kuja kuifunga simba sasa hivi anaozea yanga. Wachezaji wa bongo bangi zinawazingua.

      Delete
    2. Amwulize Tegete aliedanganywa arudi bongo kuja kuifunga simba sasa hivi anaozea yanga. Wachezaji wa bongo bangi zinawazingua.

      Delete
  12. ANAITAJI COUNCELLING ,ANAPENDA SANA KUPARUA

    ReplyDelete
  13. Ngasa ana matizo ya kichwa na yanga hawaiwezi simba hata kwa kuwachulia wachezaji, goli tano hazitafutika zipo na zitaendelea kuwepo, hawaiharibii simba maisha bali maisha ya ngassa mwenyenyewe yanaharibika, simba wamepita akina serengo , wasso, samatta, ochan na wengine wengi na simba ipo pale pale wewe ngassa ni nani harafu unaleta uongo eti unapelekwa kama mzigo wakati wewe ndio uliye toa namba za viongozi wa simba na azam kwa El melek wewe si umeshikiwa akili!

    ReplyDelete