Search This Blog

Wednesday, December 5, 2012

EXCLUSIVE: YAW BERKO KWENDA FC LUPOPO - NDUGU WA TWITE KUJAZA NAFASI YAKE YANGA



Klabu ya Yanga wapo katika hatua za mwisho za kumtoa golikipa wao wa kimataifa kutoka Ghana Yew Berko kwenda klabu ya FC Lupopo ya Congo kwa mkopo.

Kwa mujibu wa chanzo cha kuaminika kutoka Yanga ni kwamba klabu hiyo wanampeleka Berko FC Lupopo ili waweze kupata nafasi ya kumuongeza Kabange Twite katika usajili wa dirisha dogo.

Berko jana alionekana akiwa katibu wa Yanga wakiwa katika ofisi za ubalozi wa Congo wakifuatilia taratibu mbalimbali za viza ya kwenda nchini Congo kwa ajili ya kujiunga na Lupopo.

Kabange Twite
Kabange Twite inasemekana ameshamalizana na Yanga na siku chache zijazo atakuja kujiunga na timu yake mpya ili kuanza kujipanga na msafara wa klabu hiyo kwenda nchini Uturuki kwa ajili kuajindaa na ligi kuu ya Tanzania bara. 

No comments:

Post a Comment