Search This Blog

Thursday, December 27, 2012

CHRIS KATONGO ATUNUKIWA NA WANAJESHI WENZAKE ZAMBIA

Nahodha wa mabingwa wa Afrika Chris Katongo ametunukiwa na jeshi la Zambia.

Katongo, ambaye ni ofisa wa jeshi la nchi hiyo, alitunukiwa tuzo ya heshima ya jeshi la Zambia na meja jenerali Toply Lubaya katika sherehe zilizofanyika huko Arakan barracks mwanzoni mwa wiki hii.

Tuzo hii ya heshima imekuja baada ya mshambuliaji huyo wa Zambia kuchaguliwa kuwa mchezaji bora wa BBC African Footballer of the Year award. 

Jeshi la nchi hiyo pia lilitoa tuzo na maua kwa wachezaji wengine wa Chipolopolo ambao ni maofisa wa jeshi - Felix Katongo na Nathan Sinkala. 

No comments:

Post a Comment