Search This Blog

Friday, November 23, 2012

VILLAS-BOAS NA DI MATTEO - MAJENEZA YAO STAMFORD BRIDGE YALICHONGWA NA WEST BROM NA TIMU ZA SERIE A


Najua unajua kwamba Andre Villas-Boas ndiye aliyempeleka Robert Di Matteo, Chelsea, kama msaidizi wake. Kabla, Di Matteo alikuwa ni kocha mkuu wa West Bromwich Albion, huko alifukuzwa baada ya timu kufanya vibaya kwenye ligi kuu msimu wa 2010/11. Baada ya Villas-Boas kufukuzwa Chelsea, Di Matteo alitajwa kuwa kocha wa muda wa Chelsea baada ya kupata mafanikio makubwa katika muda mfupi, msimu wa 2011/12 ulipoisha, alipewa kazi ya kuwa kocha mkuu wa Chelsea kuanzia msimu wa 2012/13. Di Matteo naye sasa hivi ameshatimuliwa Chelsea.

Nataka ujue jinsi Villas-Boas na Di Matteo kufukuzwa kwao katika klabu ya Chelsea jinsi kunavyofanana;

MECHI ZAO ZA MWISHO ZA LIGI KUU NA LIGI YA MABINGWA ILIZIHUSISHA KLABU YA WEST BROMWICH ALBION NA NCHI YA ITALIA:

Andre Villas-Boas

Tarehe 21 February, 2012, Chelsea ilifungwa 3-1 na Napoli kule Italia kwenye mechi ya ligi ya mabingwa wa Ulaya. Lavezzi alifunga mara mbili na Cavani huku goli la Chelsea likifungwa na Mata.

Tarehe 4 March, 2012, Chelsea ilifungwa 1-0 na West Bromwich Albion, hii ndio ilikuwa mechi ya mwisho ya Villas-Boas, Gareth McAuley. Siku hii Villas-Boas alifukuzwa.

Roberto Di Matteo

Tarehe 17 November, 2012, Chelsea ilifungwa 2-1 na West Brom, Di Matteo, kwanza alikuwa amefungwa na timu yake ya zamani pili kwa mara nyingine Chelsea ilikuwa inafungwa kwa tofauti ya goli moja WBA. Shane Long na Odemwingie waliwaua Chelsea, Hazard aliwapatia Chelsea bao la kufutia machozi. Game ilipigwa pale pale kwenye uwanja wa WBA, The Hawthorns.

Tarehe 20 November, 2012, Chelsea inafungwa goli 3 kwa mara nyingine kwenye ardhi ya Italia huku wenyewe wakiambulia patupu safari hii, walipokuwa wakicheza dhidi ya Juventus. Quaglirella, Vidal na Giovinco. Kesho yake tarehe 21, Di Matteo alikuwa amefukuzwa.

Imeandaliwa na PodoBest

Twitter: @iPodoBest

No comments:

Post a Comment