Search This Blog

Friday, November 16, 2012

MFUPA ULIOMSHINDA DIEGO MARADONA - FILBERT BAYI HAUWEZI

Na Simon Chimbo

Akiaminika kuwa ni mchezaji bora zaidi kuwahi kutokea katika ulimwengu
  wa soka, baada ya Pele, Diego Almando Maradona alishindwa kuisaidia Argentina pale alipopewa  dhamana ya kuifundisha timu yake ya taifa.
 

Sio yeye tu, wapo wengi lakini umewahi kujiuliza kuwa kwanini Pele sio kiongozi mkubwa wa soka duniani? Na pengine sijui kama Ronaldinho Gaucho anaweza?

Hapa nyumbani Tanzania, ukimzungumzia Filbert Bayi {Kiongozi wa
Tanzania Olympic Commision TOC} pengine ni kipaji 'adimu' zaidi kuwahikutokea kwa wanamichezo wote huku Sunday Manara akiwakilisha kwa soka.

Miaka ya 1970+  Bayi aliweka rekodi adimu katika michuano mbalimbali ya riadha ikiwemo jumuiya ya Madola, All Africa Games na mingine mingi. Je hiyo ni tiketi ya yeye kuwa kiongozi bora wa TOC? Jibu wanalo Waagentina walipo muamini  Diego Maradona na kuvuna matokeo hasi.


Ndio maana haikuhitaji Sir Alex  kuwa mchezaji bora wa dunia ili
awafikishe Manchester United mahali walipo.
Uongozi ni 'committment na Accountability' au kwa maneno mengine ni wito Watanzania wanao jua hawapo kwenye system na hilo lina tutafuna hadharani.
Ni wakati wa Bayi kuwaachia wengine waende Singida na Arusha
kuwachukua wanariadha Mungu ibariki Tanzania

No comments:

Post a Comment