Search This Blog

Thursday, November 15, 2012

MATAIFA HURU YA AFRIKA: MAREFA KUFICHWA KUEPUSHA UPANGAJI WA MATOKEO

Marefa  wa fainali zijazo za kombe la mataifa huru ya Afrika watawekwa mbali na watu wengine wakati wa michuano hiyo nchini South Africa ili kuzuia upangaji wa matokeo.

Hali ya ulinzi ilitumika pia katika fainali ya za kombe la dunia mwakak 2010 zilizofanyika nchini SA.

CEO wa kamati ya ndani ya uandaaji Mvuso Mbebe alisema: "Marefa watakuwa mafichoni katika hotel mojawapo ambayo hakuna mtu atakuwa na uwezo wa kuwafikia.

"Hawatokuwa na uwezo wa kuwasiliana na mtu yoyote kutoka nje, kwa sababu hatuwezi kujua nini kinaweza kufanyika katika mawasiliano yao na watu wasioruhusiwa.

Aliongeza: "Watakuwa wanaondoka hotelini, chini ya ulinzi mkali utakaokuwa ukisindikizwa na vikosi maalum vya ulinzi, hali itaendelea mpaka mwisho wa michuano."

Shrikisho la soka la Afrika limepitisha hatua hiyo ya ulinzi wa marefa ambao utaanza kuanzia January 19 mpaka February 10

No comments:

Post a Comment