Search This Blog

Thursday, November 22, 2012

MAONI YA MDAU OMARI ISSA


HII NI KWA WADAU NA VILABU VYOTE.

Msimu uliopita 2011-2012 wa ligi kuu Tanzania Bara ilipokua imemaliza mzunguko wa kwanza tuliambiwa mzunguko wa pili ligi itaendeshwa na chombo huru(kampuni) lakini mzunguko wa pili ulipoanza hakukua na hicho kitu.Tukaambiwa ligi ya 2012-2013 itaendeshwa na chombo huru cha ajabu hadi mzunguko wa kwanza unaisha hatujaona hicho chombo huru ila tunaambiwa tena kuwa mzunguko pili league itaendeshwa na chombo huru. Sasa tujiulize je club zipo kwenye huo mchakato wa kuunda hicho chombo huru au wako busy na mambo yao tu? Je TFF wanania ya kweli kuachia ligi? Nakumbuka kuna kipindi vilabu vionyesha umoja wa hali ya juu sana na mchakato ulikua katika hatua nzuri sana cha ajabu Raisi wa TFF alivyoona umoja wa vilabu umedhamilia kufanya kweli aliamua kuuvunja umoja ule kwa kuunda kamati ambayo haina maana.Nawakumbusha vilabu na wadau muda wa mapinduzi umefika tena ya lazimaaa. Vilabu amkeni upya kwa kasi ya ajabu mnanyonywa wenyewe hamuoni au viongozi mnashiriki kuvinyonya vilabu vyenu?

No comments:

Post a Comment