Search This Blog

Friday, November 9, 2012

BREAKING NEWS! AGGREY MORRIS AONDOLEWA KWENYE KIKOSI CHA AZAM.

Baada ya leo asubuhi kutoa maoni kwa klabu ya AZAM ya kumuondoa kikosini nahodha Aggrey Morris kama kweli alihusika na tuhuma za rushwa,hatimae hivi punde nimepata taarifa kutoka kwenye chanzo cha kuaminika beki huyo na nahodha wa timu hiyo ameondolewa kwenye kikosi na kocha Stewart Hall.
Tayari Morris alikuwa mjini Tanga pamoja na kikosi cha Azam kinachojiandaa na mchezo dhidi ya JKT MGAMBO hapo kesho amerejeshwa jijini Dar Es Salaam,kocha Stewart Hall amemuondoa nahodha huyo kikosini baada ya kuonyeshwa vielelezo vya wachezaji waliohusishwa na tuhuma za kuchukua rushwa ili kuifungisha Azam, kitendo ambacho kimewaudhi sana wachezaji wa Azam.

I SALUTE YOU AZAM KTK HILI!Nawaomba kamwe msirudi nyuma it's time now kwa ajili ya kutokomeza rushwa michezoni hasa mchezo wa soka.

6 comments:

  1. Tunaomba na sisi mtuonyeshe hivyo vielelezo. Na aliyetoa hiyo rushwa naye apelekwe kwenye vyombo vya sheria. Hii tabia ikome. Watu wanatumia fedha nyingi kwenye kuandaa timu halafu kuna wengine wanatumia njia ya mkato kupata matokeo mazuri.
    Halafu cha kushangaza, kuna mitimu inatumia fedha nyingi kipindi cha usajili halafu bado inatoa rushwa ili ipate ushindi. Ajabu!

    ReplyDelete
  2. why are you saluting them, is he the only important player that did that? . from what i heard is that there two midfielders who also involved in that scandal. what abt them? by not mrntiomimg their names,it shows how weak and stupid the azam management is.. if they could mention morris, whats stopping them from mentioning the other two?.. I also questions hall's stand on this, you know two of your players took bribe to loose a game, why dont you remove them?

    my second point is on TFF.. what are they doing abt this? this is a HUGE scandal and if its proven than yanga and simba did that..what are they going to do? demote them? i dont expect these two clubs to walk free aftr this scandal if tff are real there fr the good of tanzanian football.

    i havent heard anythng from tff abt this and that is really shocking when you consider how things are run in modern football. waiting on takukuru will be useless cause at the end of the day the same things will happen again.
    i expect league officialls to loose their jobs, tff officialls and every villain on this including demotion of both yanga and simba.

    my point on yanga and simba, these two clubs havent done anythng about the allegations.. The club officialls should be tough on azam if this is not true cause clearly it has destroyed the clubs reputation. Aam also should be fined if they fail to produce enough eveidence on this,.

    reading from your previous articles on this, you have said the players including mprris have admitted on taking the bribe. i think they should be arrested cause that is criminal offense and law should take its cause.

    ReplyDelete
  3. Hao azam wapo kwenye siasa tu za mpira,waangalie walipojikwaa kuliko kuanza kila wakifungwa na simba au yanga kusingizia marefa na rushwa hizo zilikuwa siasa za mpira za simba na yanga,azam mjiingiza kichwa kichwa MMEKWISHA!!
    Pale azam inaonekana kuna mchongo upo kwa wachezaji wasiopangwa kusema wenzao wamepewa mshiko wafungwe ili nao wapate nafasi ya kucheza,haya mmeipata m perfom sasa ili tuwajue.Angalia magoli waliyo fungwa na simba ni magoli mazuri ambayo yanaonekana yamefungwa kwa kuwazidi au makosa ya kawaida ya mabeki.AZAM KWENYE MANAGEMENT WEKA WATU AMBAO WANA VISION KTK MICHEZO,SIO LEO
    MTU ALIKUWA ANASIMAMIA VIZURI ORDER ZA UNGA NA MWONGEAJI MZURI WA MPIRA UNAANZISHA TIMU UNAMBANDIKA,Hivi wadau nisaidie wapi mliona tangazo la ajira kwenye timu ya azam ambayo tuliitegemea kuleta mabadiliko ktk soka,kwenye ajira ndo watu mbalimbali utaona CV zao.

    ReplyDelete
  4. nowadays tz football is full of pilitics. it is very difficult to discern the truth even if they carry out what they call independent investigations. i doubt credibility and integrity of those making allegations as it is for the accused team (s)

    ReplyDelete
  5. Ninaunga mkono 100% kwamba kama sualal hilo lipo au kuna tetesi juu ya kutokea rushwa basi lishughulikiwe kwa mapana yake na TFF na serikali na wadau wote wa soka. kama ni kweli YANGA na SIMBA wanadaia kujihusisha na suala hili basi ufanyike uchunguzi wa kina na maamuzi yawe ya uzito unaolingana na uzito wa suala lenyewe....hata kama ni watu kufungiwa kucheza au kuongoza soka kwa uhai wao uliosaia au kama ushahidi unailenga timu kwa maana ya maamuzi ya uchafu huo kufanyika rasmi katika vyombo vyombo vya maamuzi basi timu husika( yanga, simba au nyingine yoyote) ishushwe daraja au ifutwe

    ReplyDelete
  6. Hivi azam wanayaona matendo ya rushwa pale tu wanapofungwa? Vipi msimu uliopita mechi zao nyingi zilizongwa na matukiokama hayo kwa wao kuhusishwa na udanganyifu wa namna hiyo ambapo michezo yao mingi haikuisha salama ama refa kudundwa na timu pinzani au mechi kuvunjika.

    ReplyDelete