Search This Blog

Thursday, November 15, 2012

AZAM KUSAJILI WAKENYA WATATU - KUJIIMARISHA LIGI KUU RAUNDI YA PILI NA MICHUANO YA KIMATAIFA

Katika kujiimarisha kwa ajili ya michuano ya kimataifa na ligi kuu ya Tanzania raundi ya pili, klabu ya Azam FC imetajwa kuwa katika mazungumzo na wachezaji watatu kutoka Sofapaka ya Kenya.

Taarifa za kuaminika kutoka kwa chanzo kilicho karibu na Azam ambayo wiki iliyopita  waliwasimamisha wachezaji wao wanne, Dida Munishi, Said Morad, Aggrey Morris na Erasto Nyoni kwa tuhuma za kupokea rushwa, kimesema majina ya wachezaji watatu kutoka Sofapaka ni Eugene Ambuchi Asike, James Situma na Humphrey Mieno

Wachezaji hao watatu wa kikenya inasemekana ni kocha Stewart Hall ndio aliyetoa maombi ya kusajiliwa kwa wachezaji hao ambao alifanya nao kazi wakati akiwa kocha wa Sofapaka baada ya kutimuliwa Azam FC miezi kadhaa iliyopita.

No comments:

Post a Comment