Search This Blog

Saturday, October 27, 2012

LIVE MATCH CENTRE: SIMBA SC 3 - 1 AZAM FC


Dk 90+6 MPIRA UMEISHA. SIMBA 3 - 1 AZAM
 
Dk 90+1 Kazimoto anashindwa kupiga mpira langoni kwa Azam akiwa katika nafasi nzuri.
 
Dk 90 wachezaji wa timu zote wanachezeana rafu za hapa na pale na mwamuzi anapeta.

Dk 89 mwamuzi wa akiba anaonyesha muda wa ziada kuwa ni dakika 6

Dk 87 Simba inafanya mabadilko anatoka Ngassa anaingia Edward Christopher.

Dk 85 Azam inatawala mchezo na kuishambulia Simba kwa muda mrefu.

Dk 83 Azam inapata faulo nje kidogo ya eneo la hatari la Simba na mpira unaopigwa unakuwa kona. Kona inapigwa na Azam inakosa bao la wazi baada ya mashuti ya washambuliaji wake kuwababatiza mabeki wa Simba.

Dk 82 Humud anamfanyia madhambi Okwi. faulo isiyo na madhara imepigwa.

Dk 80 Simba inafanya mabadiliko, anatoka Amri Kiemba anaingia Ramadhan Chombo aka Redondo.

Dk 79 Azam wanakosa bao la wazi bada ya Mcha kupiga kichwa amapira wa krosi uliopigwa na Shikanda. Mabeki wa Simba wanaokoa hatari hiyo na wakati huohuo beki Cholo wa Simba ameumia na anatibiwa.

Dk 76 Simba inafanya mabadiliko anatoka Sunzu anaingia Ramadhan Singano aka Messi.

Dk 75 mashabiki wanaokaa majukwaa ya upande wa Yanga wanaanza kuondoka huku wakizomewa na mashabiki wa Simba.

Dk 73 Morad anamchezea rafu Okwi nje kidogo ya eneo la hatari la Azam. Ngassa anapiga faulo na kipa Mwadin anautoa nje mpira na kuwa kona isiyo na madhara.

Dk 72 Simba inafanya shambulizi kali langoni kwa Azam lakini umakini wa mabeki unaokoa.

Dk 68 Kasim anapiga shuti hafifu kuelekea lango la Simba na kipa Juma Kaseja anadaka.

Dk 65 Simba inapata faulo, Baada ya Ngassa kuangushwa nje kidogo ya eneo la hatari la Azam, Okwi anapiga nje faulo hiyo.

Dk 64 Azam inafanya mabadiliko wanatoka Jabir Aziz na Himid Mao, wameingia Abdi Kasim na Kipre Bolou.

Dk 63 Humud anamfanyia madhambi Kazimoto
Dk 62 Mpira umebalance timu Zinashambuliana kwa zamu
Dk 58 Azam inapata faulo nje kidogo ya eneo la hatari la Simba baada ya Mcha kuangushwa na Kapombe.

Dk 53 Simba inatawala mchezo ikicheza soka la kasi sana. Azam imeelemewa.

Dk 50 GOOOO.... Okwi anaifungia Simba bao la tatu kwa shuti kali akiwa nje ya eneo la hatari la Azam baada ya kuwapiga chenga wachezaji watatu wa Azam.

Dk 49 Azam inapata kona, Beki Aggrey Moris wa Azam anakosa bao baada ya mpira wake wa kichwa kutoka nje akiunga kona.
Dk 48 Tcheche anakosa bao akiwa eneo zuri la kufunga langoni kwa Simba.

Dk 46 beki Cholo wa Simba anaumia baada ya kujigonga na mchezaji mwenzake.

Dk 46 Kazimoto anakosa bao la wazi akiwa peke ya na kipa Mwadini ambaye anaudaka mpira.

Kipindi cha pili kimeanza
17:45 timu zinaingia uwanjani
Dk. 45 HALF TIME. Simba 2 - 1 Azam

Dk 45 Sunzu anaumia baada ya kukanyagwa na bek wa Azam, Said Morad.

Dk 44 Himid Mao anamchezea rafu Amir Maftah.

Dk 43 Okwi anaichambua ngome ya Azam, lakini mabeki wa Azam wanaokoa na kuwa kona ambayo haina madhara.

Dk 41 Goooo.... Okwi anaipatia Simba bao la pili kwa kichwa akiunga krosi ya Kazimoto.

Dk 40 Kazimoto wa Simba anachezewa faulo nje kidogo ya llango la Azam.

Dk 39 Okwi anashindwa kuunganisha krosi safi ya Ngassa akiwa peke yake na kipa Mwadin wa Azam.

Dk 37 Amir Maftah wa Simba anaumia na kutibiwa. Aligongana na Ibrahim Shikanda wa Azam.

Dk 36 Ngassa anakosa bao la wazi akiwa amebaki na kipa wa Azam, Mwadin Ally. Mwadin anapangua shuti la Ngassa na mpira unafika kwa Sunzu ambaye shuti lake linaokolewa kwa kichwa na Said Moradi.

Dk 34 Mcha anakosa bao la wazi akiwa amebaki na Kaseja baada ya mabeki wa Simba kujichanganya katika kuokoa.

Dk 30 beki wa Simba, Nasoro Masoud Chollo anajigonga katika miguu ya Himid Mao na kuumia. mpira umesimama, Chollo anatibiwa.

Dk 29 Jabir Aziz anamchezea rafu Amri Kiemba wa Simba. mwamuzi Nkongo anamuonyesha kadi ya njano Jabir.

Dk 28 Okwi anaichambua ngome ya Azam lakini anapiga shuti kali nje ya lango.

Dk 27 Jabir Aziz wa Azam anapiga mpira nje baada ya kutengewa vizuri mpira na Mcha.

Dk 25 Azam ainapata kona mbili katika lango la Simba

Dk 24 Himid Mao anachezewa rafu na Jonas Mkude wa Simba

Dk 22 Azam inapata kona baada ya beki wa Simba, Ochieng kutoa nje mpira kwa kichwa.

Dk 21 Azam wanafanya mabadiliko anatoka Bocco anaingia Khamis Mcha.

Dk 19 Bocco anaanguka mwenyewe na kutibiwa katikati ya uwanja.

Dk 18 Ngassa anachezewa faulo na Himid Mao.

Dk 17 Mwinyi Kazimoto anapiga shuti kuelekea lango la Azam na mpira unatoka nje kidogo ya goli.

Dk 14 Kasi ya mpira imepungua kidogo na timu zinashambuliana kwa zamu

DK 11 Azam inapata kona baada ya Kapombe kutoa mpira nje. Kona butu inapigwa.

Dk 7 Goooo....Sunzu anaifuangia Simba kwa kichwa bao la kusawazisha akiunganisha krosi ya Mrisho Ngassa. Simba 1 - 1 Azam.

DK 6 Kipa wa Azam, Mwadin Ally anaumia na kutibiwa baada ya kugongana na Sunzu

DK 4 Gooo.... Bocco anaifungia Azam bao la kwanza abaada ya kumzidi mbio beki wa Simba Pascal Ochieng

Dk 3 KIEMBA anamwangusha Bocco nje kidogo ya eneo la hatari la Simba. bocco anapiga faulo na mpira unatoka nje

Dk 1 Amri Kiemba wa Simba anachazewa faulo nje kidogo ya eneo la hatari la Azam. Emmanuel Okwi anapiga fauloa ambayo inaokolewa na mabeki wa Azam

Mpira umeanza uwanja wa taifa Simba 0 - 0 Azam 

Mwamuzi wa leo ni Israel Nkongo

16:31 Timu zinaingia uwanjani tayari kwa kukaguliwa

Kikosi cha Simba kitakachoanza dhidi ya Azam: Kaseja, Maftah, Ochieng, Hatib, Mkude, Kiemba, Kazimoto, Sunzu, Ngassa na Okwi

AZAM FC
Ally Mwadini, Ibrahim Shikanda, Sahm Nuhu, Said Morad, Aggrey Morris, Humud, Jabir Aziz, Himid Mao, Bocco, Kipre Tchetche, Salum 

1 comment: