Search This Blog

Friday, October 19, 2012

EL HADJI DIOUF: STEVEN GERRARD NI MBINAFSI KULIKO WACHEZAJI WOTE DUNIANI - MAGWIJI WA LIVERPOOL HAWAMPENDI KWA TABIA ZAKE

Baada juzi kuiomba serikali kuwaondoa viongozi wote wa shirikisho la soka la Senegal akiwalaumu kutokana vurugu zilijitokeza kwenye mechi dhidi ya Ivory Coast, leo hii mchezaji mtukutu El Hadji-Diouf  amezungumza tena, na muda huu ametoa tuhuma kali dhidi ya nahodha wake wa zamani wa Liverpool Steven Gerrard.
Katika mahojiano L’Equipe, mshambuliaji wa Leeds alizungumzia kazi yake ya soka na tabia yake yake isiyoridhisha, lakini zilikuwa kauli zake dhidi ya Gerrard ndizo zilizoleta utamu wa mahojiano yake. Maneno ambayo kiukweli yalikuwa yanalenga kujibu mapigo ya Gerrard aliyemuandika vibaya kwenye kitabu chake kwa kumuita msenegali huyo Panya.
“Maneno ya Steven Gerrard? Ni wivu tu. Nilikuwa ndio mchezaji muhimu zaidi kwa kipindi kile, na kila mtu alikuwa akiniangalia mimi. Nilikuwa naisadia sana timu yangu ya taifa na nilifanikiwa mpaka kuipeleka katika robo fainali kwenye World Cup 2002.
“Nilikuwa kwenye listi ya wachezaji bora 100 wa karn waliotajwa na Pele na Gerrard hakuwemo. Namheshimu kama mcheza soka, lakini hakuna mchezaji mbinafsi kama yeye. Alikuwa yupo radhi Liverpool ifungwe lakini yeye afunge bao.
 ”Hajali kuhusu kitu chochote wala mtu yoyote. Nimeongea na magwiji wa Liverpool na wote wanachukizwa na tabia zake."

No comments:

Post a Comment