Search This Blog

Thursday, October 18, 2012

BAADA YA KUPIGWA BENCHI SANA - GOLIKIPA WA BARCA AGEUKIA UTENGENEZAJI MUZIKI

Baada ya kukaa becnhi kwa muda mrefu katika kikosi cha Barcelona golikipa Jose Pinto amethibitisha kupita akaunti yake ya  Twitter kwamba amesaini mkataba wa kutengeneza muziki wa bendi ya rap Delahoja.


Mchezaji huyo wa Celta amesaini mkataba huo na Sony Music Spain kusaidia kutengeneza na kulifanyia promotion kundi hilo ambalo amekuwa na ukaribu nalo kwa zaidi ya miaka 20.

"Mkataba umesainiwa (baada ya miaka 22 ya kufanya kazi ya uproduyza) na Sony Music Spain," aliandika kwa mashabiki wake 168,000 wa Twitter.

Baadhi ya vyombo vya habari nchini Hispania vimekuwa vikimtania Pinto tangu habari hizi zitoke kwamba amepata kazi ya kufanya zaidi ya kukaa kwenye benchi la Barcelona huku akimuacha Victor Valdes akitamba kwenye milingoti mitatu ya Blaugurana

No comments:

Post a Comment