Search This Blog

Friday, September 7, 2012

KALI YA LEO: NAHODHA WA MANCHESTER UNITED AKAMATWA KWA KUFANYA MAPENZI HADHARANI

Star anayechipukia wa klabu ya Manchester United ya Uingereza  amekamatwa na polisi kwa tuhuma za kuonekana akifanya tendo la ndoa na mpenzi wake hadharani.

Luke McCullough, 18, ambaye msimu uliopita alikuwa nahodha wa Academy ya United, alionekana kwenye kamera za CCTV akiwa na mwanamke wakifanya mapenzi saa 11 asubuhi baada ya kukesha usiku mzima klabu.

Mchezaji huyo raia wa Ireland amekuwa akitajwa na mabosi wa Old Trafford kama Jonny Evans mpya.

Tukio hilo lilotokea eneo la Concert Square, kwenye bar maarufu katika wilaya ya Liverpool, litamuudhi sana kocha wake Sir Alex Ferguson.

Fergie huwa na mkali sana kwa vijana wake hasa wachanga, na wiki iliyopita aliwakataza wachezaji wadogo wote chini ya umri wa miaka 23 kuendesha magari ya kifahari yanayogawiwa na mdhamani mpya wa klabu Chevrolet.

Imetaarifiwa kwamba Luke akiwa na demu wake walionekana wakiwa wapo nusu uchi huku wakifanya mapenzi, na ndipo polisi wakaenda eneo la tukio na kuwakamata.

Wapenzi hao walishatuliwa na polisi na kuonywa kisha wakaachiwa, na walipoondoka na kufika mbele kidogo wakarudia tena mchezo wao, polisi wanasema.

Maofisa wa polisi walienda tena mpaka kwenye eneo lile na kuwakamata kisha kuwapeleka kituoni na sasa wanakabiliwa na kesi ya kufanya mapenzi hadharani.

No comments:

Post a Comment