Search This Blog

Saturday, September 8, 2012

BAADA YA KUWEKEA INI JIPYA MADAKTARI WAMPA RUKSA KWA ABIDAL KURUDI UWANJANI

Mlinzi wa Barcelona Eric Abidal ameambiwa na madaktari ambao walimfanyia upasuaji wa upandikizaji wa ini kwamba hakuna sababu itakayomfanya asiendelee kucheza soka.

Mfaransa huyo aligundulika kuwa na uvimbe kwenye ini lake mwezi March 2011 na akaenda kufanyiwa upasuaji muda mfupi baadae, lakini yakatokea matatizo kidogo ya kiafya ambayo yalimlazimu awekewe ini jipya mapema mwaka huu.

"Siku zote amekuwa akiniambia anajisikia vizuri," anasema daktari Garcia Valdecasas.

"Hakuna sababu itakayomfanya asicheze tena soka, lakini kitu muhimu kabisa ni kwamba yupo hai na ana afya nzuri kabisa."

Kilichobaki sasa kwa Abidal ni kujitahidi kupunguza uzito uliotokana na kutokufanya mazoezi kwa muda mrefu kiasi cha kumfanya apate kilo 6 za ziada, lakini ili kuweza kurudi uwanjani mapema Abidal amepewa vipindi vinne vya kufanya mazoezi ya gym kwa siku, hivyo anaweza kurejea uwanjani muda wowote kutoka sasa.

No comments:

Post a Comment