Search This Blog

Friday, June 1, 2012

KUTOKA KWA PLATINI MPAKA DAVID VILLA: WATU SABA WALIOITAWALA MICHUANO YA EURO


Mastaa wengi wamewahi kung'ara kwenye michuano ya Ulaya - lakini ni wachache wameweza kutawala kama majembe haya.

Huku michuano ya nchini Poland na Ukraine ikiwa karibuni kuanza, tunachukua nafasi hii kukuletea watu saba ambao waliwasha moto wa kutisha kwenye historia ya michuano ya Euro.

MICHEL PLATINI (1984)


Mfaransa huyu  kwa sasa anajulikana zaidi kama Raisi wa Uefa mwenye sheria za utata zaidi, lakini hakuna mchezaji aliyeitawala michuano ya 1984 kama yeye.

Kiungo huyu wa aina yake alifunga mabao tisa kwenye mechi tano huku akiiongoza nchi yake kushinda ubingwa wa ulaya kwenye ardhi ya nyumbani.

Baada ya kufunga hat-tricks mbili kwenye mechi za hatua ya makundi, Platini alifunga bao kwenye dakika za nyongeza za mechi ya nusu fainali dhidi ya Ureno.

Ufaransa wakaingia fainali na kwa mara nyingine alifanya balaa kwa kupiga faulo iliyotinga nyavuni kwa kumshinda golikipa wa Spain Luis Arconada.



MARCO VAN BASTEN (1988)

 
Career ya Mholanzi iliishia njiani kutokana na balaa la majeruhi, lakini huyu jamaa alikuwa kwenye kiwango cha juu sana.

Unless, labda kama ulikuwa muingereza, baada ya timu zote mbili za mataifa haya kufungwa kwenye mechi zao za ufunguzi, mechi ya kundi B kati ya Uholanzi na England ilikuwa muhimu sana.

Van Basten akafunga hat-trickna kumsumbua sana kinda Tony Adams, wakati wadachi walipowafungasha virago England.

Mchezaji bora wa ulaya kwa mara ya tatu alienda na kufunga goli la ushindi la ushindi dhidi ya Ujerumani magharibi kwenye nusu fainali lakini balaa zaidi lilikuwa njiani.

Van alifunga bonge la bao kwenye 'impossible angle' dhidi ya Umoja wa Soviet - goli ambalo linatajwa kama moja ya mabao bora kabisa ya fainali za ulaya.

Alimaliza michuano hiyo kama mfungaji bora.


PETER SCHMEICHEL (1992)



Ulikuwa umepita mwaka mmoja tu tangu Sir Alex Ferguson alipe £505,000 kumnunua mdenmark huyu.

Denmark haikuwa hata ikitakiwa kushiriki michuano hiyo lakini walichukua nafasi ya nchi iliyokuwa kwenye vita ya wenyewe kwa wenyewe Yugoslavia na wakaweza kuwashangaza watu na kubeba ndoo ya ulaya.

Hilo liliwezekana zaidi kutokana na uwezo wa golikipa ambaye alitisha sana kwa kuzuia michomo ya hatari.

Schmeichel aliikoa mpaka penati ya Marco van Basten na kupelekea Uholanzi iliyokuwa ikipewa nafasi kubwa kutolewa kwenye mashindano katika hatua ya nusu fainali.

Hatari ya Denmark iliendelea huku Schmeichel akitoka na clean sheet kwenye ushindi wa 2-0 kwenye fainali dhidi ya Ujerumani.

ALAN SHEARER (1996)
 

Kwa kukumbuka kiangazi cha mwaka 1996, mshambuliaji huyu alikuwa akiwafanyia umafia mabeki wa pinzani    - akifunga magoli kutoka kwenye kila angle - alikuwa mshambuliaji wa kati aliyekamilika haswa.

Ndio ni rahisi kusahau kwamba alienda kwenye Euro 96 akiwa hajafunga katika mechi 12 ndani ya 21 akiwa na England.

Ingawa makelele yote aliyokuwa anapigiwa kocha Terry Venables kumtema mshambuliaji yalianza kuisha na kusahaulika mara tu alipofunga goli kwanza kwenye michuano hiyo katika dakika ya 22 dhidi ya Switzerland.

Kutoka pale akaendeleza balaa zaidi. Kwenye mechi dhidi ya Scotland na kabla ya kuwatesa sana Uholanzi kwenye mechi ambayo England iliwakandamiza wadachi 4-1 pale Wembley.

Shearer aliendeleza kufunga mabao katika mechi robo fainali England ikiwatoa Spain kabla ya kuwapa mashabiki wa England mwanzo mzuri alipofunga bao la kuongoza dhidi ya Ujerumani, ingawa England wakatolewa kwa mikwaju ya penati baada ya Gareth Southgate kukosa penati yake.

Shearer alimaliza michuano hiyo kama mfungaji bora na kubeba kiatu cha dhahabu.


ZINEDINE ZIDANE            

 
Wakati mwingine wa dhahabu wa michuano hii kwa Ufaransa ulihitimishwa na David Trezeguet.
Lakini wakitoka kushinda kombe la dunia miaka miwili nyuma, michuano hiyo iliyofanyika kwenye ardhi za Uholanzi na Ubelgiji ilimpa nafasi Zidane nafasi ya kuweka heshima zaidi kwamba ndio mchezaji bora wa wakati wake.

Wakisikia kelele za mwangi za ushindi wa akina Platini miaka 16 nyuma, Zidane akafunga bao kwenye extra time dhidi ya Ureno katika nusu fainali ya aina yake - kwa mkwaju wa penati.

Zidane alikuwa akitimiza miaka 30 siku tisa kabla ya fainali na akapokea zawadi ya siku ya kuzaliwa kwa kutajwa na UEFA kama mchezaji bora wa michuano hiyo.



OTTO REHHAGEL (2004)

 
Shujaa aliyekuwa hategemewi, mjerumani, ambaye sasa ana miaka 73, akawa mungu wa soka nchini Ugiriki  baada ya kuiongoza nchi hiyo kwenye kubeba kombe mwaka 2004

Akiwa bingwa wa kuunda ukuta wa kupaki basi golini chini ya nahodha, Theo Zagorakis kutoka Leicester City, Rehhagel alifanya maajabu mwaka 2004.

Aliiongoza timu yake kupita kwenye hatua ya makundi huku wakishinda mechi zote kwa ushindi wa 1-0 - hata ushindi wa fainali dhidi ya Ureno ulikuwa wa goli 1-0 dhidi ya wenyeji.

Siri ya mafanikio? Nyuma ya kila kocha aliyefanikiwa kuna mke mzuri wa kocha huyo na mama watoto wa Otto, Beate, ameripotiwa huwa anaenda kufanya scouting kwa wapinzani kwa ajili ya mumewe.

DAVID VILLA 2008

 
Ilikuwa ni michuano ambayo wahispania waliweka heshima baada ya kutaniwa kama warembaji kwa muda mrefu - lakini kipaji cha ajabu cha David Villa kiliiongoza Spain kujenga heshima mpya.

Mshambuliaji wa Valencia tayari alikuwa ameshafunga mabao 6 kwenye hatua ya kufuzu na akafungua michuano kwa kufunga hat-trick dhidi ya Russia.

Huku akiwa anamfunika patna wake mshambuliaji mpya wa Liverpool Fernando Torres, Villa then akafunga goli la muda wa majeruhi katika mchezo wa pili dhidi ya Sweden.

Alipumzishwa kwenye mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi, na akarudi kwenye robo fainali na akafunga bao la penati kwenye hatua ya mikwaju ya penati dhidi ya Italia na kuisadia timu yake kufika nusu fainali.

Alipata maumivu kwenye nusu fainali na akashindwa kupata nafuu kucheza mchezo dhidi ya Ujerumani ambao Fernando Torres akafunga bao la ushindi dhidi ya Ujerumani na kuwapa ubingwa Spain - huku David Villa akiibuka mfungaji bora wa michuano.


JE MWAKA HUU NANI ATAITAWALA  MICHUANO YA 2012.

1 comment: