Search This Blog

Friday, June 22, 2012

KOLO TOURE AFUNGA NDOA NA MAMA WATOTO WAKE

Mlinzi wa Manchester City Kolo Toure amefunga ndoa na mchumba wake wa siku nyingi na mama wa watoto wake wawili Chimene Akassou siku ya Alhamisi katika mji mkuu wa Ivory Coast - Abdijan, kwenye sherehe iliyowakutanisha watu tofauti kutoka kwenye matabaka tofauti kuanzia kwenye michezo mpaka wanasiasa.

Harusi hiyo imefanyika kwenye msikiti na itaendelea jumamosi ambapo Kolo na mkewe watasaini vyeti vya ndoa kiserikali.

Pia kutafanyika reception ya hatari sana wikiendi hii, huku wageni wengi wakitegemewa kuwa ni wachezaji wa timuya taifa ya Ivory Coast.

Ndugu wa Kolo, na mchezaji mwenzie kwenye klabu na Taifa, Yaya Toure alikuwa ndio best man.

Wanandoa hao wapya wamekuwa wakiishi pamoja Uingereza tangu mwaka 2003, mwaka mmoja baada ya Kolo Toure kuhamia Arsenal akitokea Asec Mimosas.

No comments:

Post a Comment