Search This Blog

Thursday, June 28, 2012

FIESTA SOCCER BONANZA SAFARI HII KUANZIA MKOANI MBEYA!

Lile bonanza lililoteka nyoyo za mashabiki wa vilabu mbali mbali vya soka barani ulaya la Fiesta Soccer Bonanza linataraji kuanza mwishoni mwa juma hili pale Mkoani Mbeya.

Bonanza hilo ambalo mwaka huu litashirikisha mashabiki wa vilabu vya MANCHESTER CITY,MANCHESTER UTD,CHELSEA,ARSENAL NA LIVERPOOL toka nchini England,kutoka nchini Hispania mashabiki wa vilabu vya REAL MADRID na FC BARCELONA pia watashiriki bonanza hili litakalofanyika kwenye viwanja vya Chuo cha Uhasibu hapo siku ya Jumapili tarehe 1/7/2012.


KUTOKA MAKTABA: mwaka jana mabingwa wa Fiesta Soccer Bonanza walikua ni mashabiki wa klabu ya INTER MILAN ya nchini Italia. JE NANI ATAIBUKA KIDEDEA WA FIESTA SOCCER BONANZA MWAKA WA 2012 HUKO MOANI MBEYA ?
Mchezaji Mwaikimba (kushoto) wa timu ya mashabiki wa Inter Milan akipokea kombe la ushindi kutoka kwa meneja wa kinywaji cha Serengeti Lager Allan Chonjo, mara baada ya mchezo wa fainali kumalizika katika viwanja vya chuo cha uhasibu (TIA) jijini Mbeya leo jioni.
Tamasha la Mwendelezo wa Dhahabu na Serengeti Fiesta Soccer Bonanza limefanyika leo jijini humo, kwenye uwanja wa Chuo cha Uhasibu (TIA), tamasha lilikuwa limechagamka sana na mashabiki wamejitokeza kwa wingi na kumekuwa na upinzani mkubwa kati ya timu za mashabiki zinazokutana kwenye uwanja huo. Dalili zilionyesha mapema kwamba huenda tamasha hilo lingevunja rekodi kwa matamasha yaliotangulia katika mikoa ya Dar es salaam, Mwanza, Dodoma na sasa Mjini Mbeya jambo ambalo limedhihirika mara baada ya kuhudhuriwa na mashabiki wengi tena waliochangamka sana.
Wachezaji wa timu ya mashabiki wa klabu ya Inter Milan ya Italia wakiwa katika picha ya pamoja na kombe lao mara baada ya kuibuka mabingwa wa tamasha la Serengeti Fiesta Soccer Bonanza

Wachezaji wa timu ya Inter Milan na Real wakiwania mpira wakati wa mchezo wa fainali katika tamasha la Serengeti Fiesta Soccer Bonanza.
Umati Mkubwa umehudhuria katika tamasha hilo ambapo kulikuwa na kila shamrashamara za mashabiki wa vilabu hivy kutoka Ulaya.
Mchezaji wa timu ya mashabiki wa klabu ya Shafii Dauda Inter Milan ya Italia (kulia) akichuana na mchezaji wa mashabiki wa klabu ya Real Madrid ya Hispania,
Hapa nilikua nikitoa maelekezo, kwa wachezaji wa timu za mashabiki wa Real Madrid na Inter Milan kabla ya kuanza kwa mchezo wao.
Meneja wa kinywaji cha Serengeti Lager Allan Chonjo akiwaelekeza jambo mashabiki wa timu ya Liverpool ya Uingereza, wakati walipokuwa wakipiga picha kabla ya kuanza kwa bonanza hilo.

Mashabiki wa timu ya Inter MilaN wakati wa kupiga na timu yao.
Hawa ni mashabiki wa timu ya mashabiki wa Manchester United kabla ya kuanza bonanza hilo.
Hii ni timu ya mashabiki wa klabu ya Arsenal ya Uingereza
Hii ni timu ya mashabiki wa klabu ya Real Madrid ya Uhispania.
Hii ni timu ya mashabiki wa klabu ya Chealsea ya Uingereza wakiwa tayari kwa gemu lao.
Hii ni timu ya mashabiki wa klabu ya Barcelona ya Hispania kama kawa.
Hapa timu zote zikishiriki maandamano kutoka katika stendi ya mabasi ya Kabwe Mwanjelwa mpaka viwanja vya chuo cha Uhasibu (TIA).
Kikundi cha matarumbeta kilichoongoza mandamano hayo kutoka mwamelwa mpaka eneo la Mafiati mjini Mbeya.
Mashabiki wa Inter Milan wakishoo Love kwa staili ya aina yake.
Wazee wa Emirates mjini Mbeya nao walikuwepo kama unavyowaona katika picha.
Mashabiki wa timu mbalimbali wakishagilia wakati wa maandamano ambayo yalianzia katika kituo cha mabasi ya Kabwe Mwanjelwa na kuishia katika uwanja wa Chuo cha Uhasibu Mbeya (TIA)

No comments:

Post a Comment