Search This Blog

Saturday, May 19, 2012

ZANTEL MDHAMINI MPYA WA BONGO STAR SEARCH


Makamu wa Rais wa Kampuni ya Etisalat, Ahmed Mokhles akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na kampuni yao kudhamini shindano la kusaka vipaji la Bongo Star Search, kulia kwake ni mkurugenzi wa Benchmark Productions iyoandaa shindano hilo, Rita Poulsen.
Shindano la BSS mwaka huu litajulikana kama ‘Epiq Bongo Star Search’  ambapo mshindi atanyakua shilingi milioni 50,pamoja na zawadi nyingine kutoka Zantel, sambamba na mkataba wa kurekodi ili aweze kuendeleza kipaji chake baada ya shindano hilo. Aidha, mchakato wa mwaka huu utawahusisha washiriki kutoka  mikoa nane tofauti ikiwemo Zanzibar, Lindi, Mbeya, Mwanza, Arusha, Tanga, Dodoma na Dar es Salaam ambapo mchakato utaanza mwezi Juni.

No comments:

Post a Comment