Search This Blog

Saturday, May 19, 2012

NIMEKUTANA NA WAKONGO HAPA: WATHIBITISHA TIKETI KUUZWA EURO 1500-2500 LEO HII

Kama ambavyo niliripoti muda mfupi uliopita kuhusu upatikanaji wa tiketi kwa ajili ya kuangalia fainali ya champions league zilivyo ghali na shida kupatikana - jioni hii nikiwa kwenye matembezi yangu nimekutana na jamaa wawili raia wa Kongo ambao wamekuja hapa Munich kwa madhumuni ya kuangalia mtanange wa kesho kati ya Chelsea na Bayern Munich. Wakongo hawa wamenithibitishia kwamba ni kweli leo kuna baadhi ya sehemu ambazo ni chache sana zimebakiwa na tiketi lakini wanauza kwa EURO 1500 -2500 ambazo ni tiketi za hadhi ya juu.



No comments:

Post a Comment