Search This Blog

Thursday, May 24, 2012

JUMA KASEJA NAHODHA MPYA TAIFA STARS



NDOTO za mlinda mlango namba moja Tanzania, Juma Kaseja kuwa Nahodha wa timu ya taifa, zimetimia baada ya benchi la ufundi la Taifa Stars, kumteua kipa huyo wa Simba SC kushika wadhifa huo.
Maofisa wa benchi la ufundi la Stars, chini ya kocha Kim Poulsen, Wasaidizi wake, Sylvester Marsh na Juma Pondamali kwa pamoja na Meneja Leopold Mukebezi, baada ya kikao chao wamemteua rasmi Kaseja kuwa Nahodha wa timu hiyo, akirithi mikoba ya beki wa kulia, Nsajigwa Shadrack ambaye ameachwa kwenye kikosi hicho.
Hata hivyo, haijafahamika kama Kaseja atakuwa Nahodha wa kudumu wau muda wa Stars, kwa sababu chini ya Jan Poulsen, aliyekuwa kocha wa Taifa Stars kabla ya Kim, Shaaban Nditi ndiye aliyekuwa anapewa mikoba ya Unahodha Nsajigwa anapokuwa nje ya kikosi.
SOURCE:http://bongostaz.blogspot.com/

No comments:

Post a Comment