Search This Blog

Thursday, May 10, 2012

JULIO: HAKUNA KAMA MILOVAN NA KIM POULSEN

Kocha Jamhuri Kiwhelu akizungumza na EXCLUSIVELY na http://www.shaffihdauda.com/ amesema makocha Milovan Cirkovic wa Simba pamoja na Kim Poulsen wa timu ya Taifa ya vijana ndo makocha pekee wenye uwezo wa kufundisha soka miongoni mwa makocha wazungu waliofanikiwa kufanya kazi hapa nchini.
pamoja na kuwasifia makocha hao Jamhuri maarufu kwa jina la Julio hakusita kumpa sifa za kipekee kocha wa timu ya taifa ya vijana mdenish Kim Poulsen kuwa ndiye kocha bora mzungu miongoni mwa makocha wote wazungu waliowahi kufanya kazi hapa nchini. 
Pia Julio ameliomba shirikisho la soka nchni kumtumia Kim Poulsen kama kocha mkuu katika timu ya taifa ya wakubwa ili kuweza kuiwezesha timu ya taifa kupata mafanikio kwa kuwa ni kocha ambaye anaipenda kazi na kuiheshimu na uwezo mkubwa wa kufundisha soka.
 

No comments:

Post a Comment