Search This Blog

Saturday, May 19, 2012

HAPA NDIPO PATAKAPOAMUA BINGWA WA CHAMPIONS LEAGUE 2012 - ALLIANZ ARENA - IJUE HISTORIA YAKE.

Allianz Arena ni uwanja wa kuchezea soka uliopo kusini mwa Munich, Bavaria - Ujerumani. Huu ni uwanja unaotumiwa na timu mbili za mji wa Munich FC Bayern Munich na TSV 1860 Munchen kuchezea mechi zao za nyumbani kuanzia msimu wa 2005-06. Timu mbili zote zilikuwa zikicheza mechi zao za nyumbani kwenye uwanja wa Munich Olympic tangu mwaka 1972. Allianz Arena ni uwanja wa tatu kwa ukubwa nchini Ujerumani nyuma ya Signal Iduna Park mjini Dortmund na Olympiastadion mjini Berlin. Uwanja huu ulifunguliwa mwaka 2005, mwezi Mei 30. Ulijengwa kwa na gharama zisipungua Euro million 340 na kampuni ya Allianz ambayo wana haki ya kutumia jina lao kwenye uwanja huo kwa miaka 30. Uwanja una uwezo wa kuingiza watu 69,901.

No comments:

Post a Comment